Thursday, March 13, 2014

WALIONUNUA IPTL SASA WAFUNGUKA.





Dar es salaam. Sakata la ununuzi wa mitambo ya kufua umeme ya IPTL, limeibuka katka sura mpya baada ya ya kampuni ya Pan Africa Power Solution  Ltd (PAP) kutetea ununizi huo.

Mwenyekiti mtendaji wa PAP Harbinder Singh Seth aliibuka juzi mbele ya wandishi wa habari akisema ununuzi wa mitambo hiyo ilikuwa biashara safi isiyokuwa na tatizo lolote kwa kuwa alifuata sheria  na kanunu husika.

“Nilifuata taratibu zote, sikuja Tanzania kuchuma fedha, ninataka kuisaidia Tanzania kupata umeme wa uhakika ambao ni muhimu kwa ukuaji  wa uchumia amesema seth.


Jumatatu iliyopita Fahari News iliripoti kwamba kati ya Novemba 28 na desemba 8 mwaka jana  PAP ilikabidhiwa dola za amrekani 122 milioni (Sh 201 bilioni) zilizokuwa katika akaunti ya Escrow  katika benki kuu ya Tanzania (BOT)

Akaunti hiyo ilifunguliwa BOT ili kuhifadhi fedha ambazo Tanesco ilistahili kulipa IPTL  kama gharama za uendeshaji , bbad ya kutokea mgogoro ambao ulizalimisha peande  husika kupelekana mahakamani .

Wiki iliyopita Fahari News  iliandika kwamba fedha hizo zilitolewa baada ya serikali kuamua kumaliza shauri hiyo na hapo ndipo fedha hizo zilipochukuliwa katika akaunti hiyo ya PAP.

Hata hivyo, pamoja na seth kukubali kuchukua fedha hizo amesema fedha zilikuwamo ni sh 150 billioni, huku akitetea hatua hiyo ya ununizi wa IPTL  kwamba siyo kinyumbe cha sheria.

Kabla ya kuuzwa PAP, IPTL ilikuwa inamilikiwa kwa ubia kati ya mechmar corporation ya Malaysia (asilimia 70) na  VIP  Engineering na Marketing  Company limited  ya Tanzania iliyokuwa na asilimia 30 .

PAP ni kampuni ya tatu katika mgogoro huo kujitokeza na kutoa ufafanuzi tangu habari zake zilipoanza kuandikwa. Kampuni ya kwanza ilikuwa ni VIP Engineering ya James Rugemalira na baadaye akaibuka mwanasheria wa IPTL na wote walitetea  mauzo hayo.

PAP ilivyonunua IPTL
Wakili wa PAP joseph mwakandege alisema kwa miaka mitano ya IPTL iliendeshwa bila kuwapo kwa mgogoro lakini baadaye iliibuka mivutano miongoni mwa wanahisa iliyosababisha kufunguliwa kwa akaunti ya Escrow.

Mwakandege alisema 2010, sethi aliwasilisha nyaraka mahakamani kuonyeshakwamba alipewa mamlaka ya kusimamia mali zote za mechamar hapa nchini.

Amesema baadaye sethi alinunia hisa zote ambazo awali mechmar alikuwa ameuza kwa piperlink na kuzihamishia PAP.

Kwa mujibu wa wakili huyo, sethi baadaye alinunua asilimia 30 zilizosalia, na tayari mmiliki wa VIP, Rugemalira amekwishakiri kupokea  dola za marekani 75 milioni (sh 120 bilioni) alizoziita kuwa ni fedha za ugoro.

Amesema baada ya mauzo hayo, VIP ilikwenda mahakamani na kuomba kesi zote zinazohusu  kampuni hiyo ya mechmar zifutwe.

September 5, mwaka jana mahakamani iliamua kufuta kesi hizo hivyo PAP akapata haki ya mumiliki mali zote za IPTL, ikiwa ni pamoja na fedha zilizokuwa katika akaunti ya Escrow.

Mwakandege alisema baada ya uamuzi huo, PAP ilikubali kulipa madeni yote ya IPTL na ufilisi wa muda uliokuwa umewekwa  kwa kampuni hiyo iliondolewa.

Kutokana na hali hiyo ilibidi kusainiwa mkataba kati ya IPTL na serikali kupitia  wizara ya nishati  na madini ifahamike kwamba akaunti ya Escrow ilikuwa mali ya wanahisa wa IPTL  haikuwa na fedha walipokodi  wala fedha za Benki ya Standard Chartered  ya Hong Kong (Mkopeshaji wa IPTL) alisema mwkandege.

Alifafanua kuwa, serikali ilitaka PAP kusaini makubalino kwamba iwapo watatokea wadai kwapya wa IPTL itawalipa. Amesema baada ya hapo serikali  aliandika barua kwa BOT kuitaka iruhusu fedha hizo zilipwe kwa PAP.  

0 Responses to “WALIONUNUA IPTL SASA WAFUNGUKA.”

Post a Comment

More to Read