Tuesday, March 18, 2014
WASOMI, WAJUMBE WATOFAUTIANA KUHUSU MZOZO WA KANUNI.
Do you like this story?
Hatua ya baadhi ya wajumbe wa Bunge Maalumu
la Katiba kupiga kelele na kulivunja jana wakipinga uvunjaji wa kanuni,
imepokewa kwa hisia tofauti na baadhi ya wasomi na wanaharakati, huku baadhi
wakisema ilikuwa ni sahihi na wengine wakipinga.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk
Haji Semboja amesema kitendo hicho ni matokeo ya kutokufuatwa kwa kanuni na
taratibu.
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kanuni ya
Bunge hilo, Profesa Costa Mahalu alishauri kuitwa haraka Kamati ya Bunge
Maalumu la Katiba ili kunusuru vikao vya Bunge hili kuendelea.
Akizungumza baada ya kuvunjika kikao hicho
jana jioni, Profesa Mahalu alisema hoja ya kuwa Mwenyekiti Sitta amevunja
kanuni kwa kuanza kumpa nafasi Jaji Warioba badala ya kuanza na Rais Kikwete
zitamalizwa kwa mazungumzo.
Profesa Mahalu alikiri kuwa kanuni
zilizopitishwa ziliweka utaratibu, lakini akasema kwa kuwa suala la kanuni ni
la kisheria, kila mtu anaweza kuwa na tafsiri yake.
“Kwa mazingira haya, siwezi kusema nani ana
makosa kwani kila mtu anavutia kwake, lakini muhimu hapa ni kukaa na kufikia
maelewano,” amesema.
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Muda wa Bunge hilo,
Pandu Amir Kificho alipotakiwa kuelezea hatua zitakazochukuliwa baada ya Bunge
kusitishwa, aliomba kupewa muda kwa sababu jambo hilo ni zito na walikuwa
wakienda kwenye vikao.
Kwa upande wake, Dk. Hamidu Shungu wa UDSM
aliwapongeza wajumbe kwa hatua hiyo akieleza kwamba wamefanikiwa kuzuia jambo
hilo.
“Wajumbe walikuwa sahihi kwa kuwa Rais ni mkuu
wa nchi anapohutubia mahali kama hapo, hiyo pia inatafsiriwa ndiyo uzinduzi,
sasa Jaji Warioba kuwasilisha hiyo rasimu kabla Bunge halijazinduliwa inakuwa
na maana tofauti,” alisema Dk. Shungu.
Alidai kwamba hatua hiyo ya wabunge imezuia
mambo ambayo labda yalikusudiwa na ambayo pengine yangeegemea kwa kile
anachokiamini au kukitaka Rais, hivyo kubadili mawazo ya wajumbe.
Sitta hakuwa tayari kuzungumzia utata
uliojitokeza baada ya msaidizi wake kuomba waandishi wa habari kutokumhoji.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “WASOMI, WAJUMBE WATOFAUTIANA KUHUSU MZOZO WA KANUNI.”
Post a Comment