Tuesday, March 18, 2014
APOKEA JENEZA LENYE MZOGA WA PAKA.
Do you like this story?
Familia
ya Bwana Oganda inasema kuwa sio mara ya kwanza kwa kisa kama hiki kuikumba
Familia
ya afisaa mmoja wa Elimu nchini Kenya imepigwa na butwaa baada ya kupata jeneza
dogo likiwa limewekwa kwenye mlango wao mjini Kisumu Magharibi mwa Kenya.
Kwa
mujibu wa taarifa ya gazeti la Taifa Leo, familia ya Afisaa huyo Elias Oganda,
mwenye umri wa miaka 56, ilipata jeneza hilo dogo likiwa na mzoga wa Paka nje
ya mlango wao na sasa inaishi kwa hofu kubwa.
Afisaa huyo anayefanya kazi katika wizara ya elimu, alisema
kuwa hii ni mara ya nne katika miezi sita kupata jeneza kama hilo nyumbani
kwake.
Polisi walifungua jeneza hilo na kupata mzoga wa Paka ndani yake. Walishuku kuwa Paka huyo alinyongwa na kuwekwa ndani ya jeneza hilo kwani hapakuwa na daVisa vingi kuhusu Paka bila shaka huwa ni vya kuogofya
Afisaa mkuu wa polisi katika eneo hilo amesema kuwa hili sio
tukio la kwanza kushuhudiwa katika eneo hilo.
Bwana Oganda naye alisema kuwa jeneza hilo liligunduliwa na mkewe Joyce Oganda, mwenye umri wa miaka 50, usiku wa manane alipotoka nje kujisaidia.
''Nia ya mtu aliyefanya kitendo hicho haijulikani, mimi sijawahi kuhusika na mzozo wa ardhi'' amesema bwana Oganda aliyeongeza kuwa familia yake haijwahi kupata utulivu kwa mwaka mmoja uliopita kwani amekuwa akifanyiwa uchawi mara kwa mara.''
''Hii ni ardhi ya babangu na sielewi kwa nini watu wanataka kunitishia maisha kwa kutumia uchawi.''
Wakazi walikita kambi katika nyumba ya bwana Oganda kushuhudia mchawi aliyeletwa katika nyumba hiyo kutoka Sirare mpakani mwa Kenya na Tanzania kujaribu kujua ni nani aliyehusika na kitendo hicho.lili yoyote ya damu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “APOKEA JENEZA LENYE MZOGA WA PAKA.”
Post a Comment