Wednesday, April 23, 2014
MABWENI YA SHULE YA SEKONDARI YA IVUMWE MBEYA YATEKETEA KWA MOTO.
Do you like this story?
Baadhi ya wanafunzi wakijaribu kutafuta madaftari yao |
Baadhi ya vitu nya wanafunzi vilivyo okolewa |
|
|
Bweni Moja la Wavulana lenye vyumba zaidi
ya Sita katika shule ya Wazazi Sekondari ya Ivumwe
inayomilikwa na Chama Cha Mapinduzi limeteketea kwa moto.
Tukio hilo limetokea leo April 23 majira ya saa3
asubuhi jijini Mbeya wakati wanafunzi hao wakiwa madarasani
kuendelea na masomo yao kama kawaida.
Akizungumza katika eneo la Tukio hilo Mwenyekiti wa
Bodi ya Shule hiyo Daktari Victory Kanama amesema kuwa moto huo umeanza majira
ya saa3 asubuhi wakati tayari wanafunzi wakiwa madarasani.
Amesema taarifa za kuungua kwa moto huo zilitolewa na
mmoja wa wananchi waliokuwa wakipita pembezoni mwa Mambweni hayo ambapo katika
maelezo yake alieleza kuwa ameona moshi mkubwa ukitokea ndani ya mabweni hayo.
Amesema mara baada ya kupata habari hizo
walitoa taarifa kwa kikosi cha zimamoto ambacho kilifika mara moja
na kuanza juhudi za kuuzima moto huo.
Amesema pamoja na kikosi hicho cha zimamoto kufika
shuleni hapo mapema na kuzima moto huo lakini tayari moto huo ulikwisha
teketeza asilimia kubwa ya mali zilizomo katika mabwani hayo.
Amesema kwa kiwango kikubwa vitu vingi vimeteketea kwa
moto huo hususani vitanda na magodoro ambayo ndiyo yaliyoungua
vibaya pamoja na vitu vingine vya wanafunzi hao.
Aidha kwa mujibu wa Daktari Kanama hakuna mwanafunzi
yoyote aliye poteza maisha kutokana tukio hilo licha ya mmoja wa wanafunzi
kujeruhiwa mkononi na kitu kinacho dhaniwa kuwa ni kioo katika harakati za
kuokoa vitu ambapo tayari amekwisha fikishwa hospitali kwa ajili ya kupatiwa
matibabu.
Aidha kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi
wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Mbeya Ndugu Fatma Asenga amesema mabweni
hayo yalichukua jumla ya wanafunzi 160 ambao ni wavulana huku chanzo cha
moto huo kikiwa bado hakijajulikana.
Amesema kwa sasa juhudi zinazofanyika na Chama
kwa kushirikiana na uongozi wa shule hiyo ili kuangalia uwezekano wa
haraka wa kuwahifadhi wanafunzi hao.
Amesema litatengwa darasa moja kwa muda ambalo
litatumika kama bweni wakati wakiendela kufanya utaratibu mwingine.
Mwisho.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MABWENI YA SHULE YA SEKONDARI YA IVUMWE MBEYA YATEKETEA KWA MOTO.”
Post a Comment