Tuesday, March 18, 2014
JK ABEBA SIRI NZITO BUNGE LA KATIBA.
Do you like this story?
Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania |
Rais Jakaya Kikwete anatarajia kuhutubia bunge maalumu
la katiba ijumaa ya wiki hii huku
akitarajiwa kuzungumzia masuala mbalimbali
ikiwemo mvutano uliojitokeza
kuhusu namna ya kupiga kura na muundo wa serikali.
Akitoa tangazo hilo jana mwenyekiti
wa bunge hilo Samuel sitta amesema Rais ameona
ni busara kulihutubia siku hiyo
kabla ya rais kuhutubia Bunge kuanzia
leo wajumbe watakuwa na semina ya siku nne kuhusu mambo mbalimbali ikiwemo historia ya muungano.
Kwa siku ya jumanne (Leo)
kutakuwa na semini kuhusu kanuni zetu za bunge ambazo zitatolewa ufafanuzi na wanasheria wetu wa serikali na pia nitateua wajumbe
wengine watatu kutoka katika kamati ya
kanuni kwa ajili ya kutoa ufafanuzi amesema.
Ameseme kesho na
keshokutwa kutakuwepo na wajumbe watatu kutoka bara na watatu kutoka Zanzibar wenye uelewa kuhusu muungano ambao watatoa
mada kuhusu historia ya muungano.
Wajumbe hawa watatueleza
historia ya muungano toka tulipotoka
hadi hapa tulipofikia ili wajumbe
wawe na uelewa mpana kuhusu muungano ,
alisema sittta.
Aidha amesema ndani ya
siku hizo pia wajumbe wawili kutoka
Kenya watatoa mada kuhusiana na uzoefu wao katika mchakato wa kutengeneza katiba ambao nchi hiyo imeupitia.
Pamoja na bunge hilo kupitisha
kanuni za bunge maalumu lakini wameshindwa
kupitisha vifungu vya 37 ana 38
ambavyo vinaelekeza namna ya kupiga kura katika kufanya maamuzi huku
wajumbe wengi kutoka vyama vya upinzani
wakitaka ya siri na CCM ikitakaya wazi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “JK ABEBA SIRI NZITO BUNGE LA KATIBA.”
Post a Comment