Tuesday, March 18, 2014
GAVANA NDULLU: FEDHA ZA IPTL ZILIFUATA TARATIBU.
Do you like this story?
SAKATA la malipo ya
kampuni ya kufua umeme ya independent
power Tanzania Ltd.(IPTL) limechukua sura mpya, baada ya Benki Kuu ya Tanzania(BoT) kuibuka na
kuvunja ukimya na kusema haiwezekani
kuzuia wala kuhoji miamala ya
fedha za akaunti maalum ya Tegeta
Escrow kwa sababu zilifuata
taratibu zote za kisheria.
Katika ufafanuzi wake kwa
waandishi wa habari jijini dare s salaam
jana Gavana wa Benki kuu Profesa Beno Ndullu amesema kuwa malipo hayo
yalitolewa kihalali na hakuna
udanganyifu wowote uliofanyika.
Amesema benki hiyo
inawajibika kisheria kutunza fedha hizo
kutokana na makubalino ya kisheria
yaliyowekwa kati ya serikali
kupitia wizara ya nishati na
madini na kampuni ya IPTL mwaka 2006.
BOT ilitekeleza majukumu
yake ya kulipa miamala ya fedha kwa
kampuni ya kufua umeme ya IPTL kwa sababu makubalino hayo yalifuata taratibu za kisheria kati ya serikali kupitia wizara ya nishati na
madini na kampuni hiyo.
Katika ufafanuzi huo amesema
kazi yao ni kuhakikisha wanatunza fedha hizo na kuzitoa kutokana na mkataba wa
kisheria uliowekwa baina ya
wahusika hao ambao ni serikali na IPTL
yenyewe.
Kutokana na hali hiyo BOT ilitekeleza makukumu yake ikijua
kuwa jukumu la msingi na la asili ni
kulipa deni hilo pale inapotakiwa kufanya hivyo yaani payment
on demand.
Amesema katika mazingira
kama hayo demand ilifanyika pale wahusika
yaani serikali na IPTL walipotekeleza matakwa ya kfungu cha 7.7 cha makubaliano ya ufunguzi wa akaunti hiyo ya tegeta Escrow.
Kwa hali hiyo mwaka
2013 wahusika hao wawili walisaini
makubaliano ya kutoa fedha zilizomo katika akaunti hiyo ili zilipwe kwa IPTL
jambo ambalo walilitekeleza.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “GAVANA NDULLU: FEDHA ZA IPTL ZILIFUATA TARATIBU.”
Post a Comment