Tuesday, March 18, 2014
DAKIKA TATU ZA WARIOBA MBELE YA MIMBARI YA BUNGE.
Do you like this story?
Mwenyekiti wa Tume ya
mabadiliko ya katiba, jaji joseph warioba jana jioni alisimama kwa dakika tatu
mbele ya kipaza sauti lakini akashindwa
kuwasilisha rasimu ya katiba kutokana
na vurugu zilizojitokeza bungeni.
Vurugu hizo zilitokea muda
mfupi baada ya mwenyekiti wa bunge hilo Samuel sitta kumwalika kuwasilisha
rasimu ya kativa kwa muda wa dakika 120.
Jaji warioba alisimama
kwenye mimbari ya bunge saa 11:02 jioni tayari kuhutubia lakini kabla ya
kufanya hivyo wajumbe kadhaa walisimama
na kuomba mwongozo wa mwenyekiti.
Waliosimama ni profesa
Ibrahimu Lipumba, james mbatia,freeman mbowe, na tundu lisssu..
Hata hivyo sitta
aliwanyima fursa akisema hakuna mwongozo hapa naomba mwenyekiti uendelee , waheshimiwa wabunge hakuna mwongozo naomba mwenyekiti uendelee
kwa ajili ya hansard .
Kauli hiyo ilionekana
kuchafua hali ya hewa kwani jaji warioba alipowasha kipaza suti tayari kuanza kuhutubia baadhi ya wajumbe walianza kupiga
kelele wengine makofi na kugonga meza hivyo kumfanya ashindwe kufanya kazi
hiyo ya uwasilishaji.
Waliokuwa mstari wa mbele
kupinga jaji warioba kuwasilisha rasimu
ya katiba kwa sehemu kubwa walikuwa ni wajumbe wanaounda kundi la umoja wa kativa ya wananchi(ukawa)
Jaji warioba akiwa
anatafakari mble ya miambari sita aliwasha kpaza sauti na kumtaka aendelee kuwasilisha rasimu ya
katiba … endelea mwenyekiti endelea kwa
ajili ya kumbukumbu rasmi(hansard)
Lissu akisikika
akijibu kauli hiyo akisema fuata kanuni mwenyekitu fuata
kanuni mwenyekiti huku akipiga kelele na kugonga meza na wakati
huo profesa lipumba akiwa amewasha kipaza sauti chake kutaka kuzungumza huku naye akiendelea kupiga meza kwa nguvu.
Wengine waliosimama na
mchungaji Christopher mtikila, Ezekiel oluoch, philimon ndesamburo, moses
machali na mchungaji peter msigwa.
Katika tatu
zilikatika huku kukiwa hakuna dalili za
hali kutulia na kuona hivyojaji warioba aliamu kuondoka kwenye miambari na
kuketi kimya akiwa na makamu mwenyekiti
wake jaji augustino ramadhani.
Baada ya hapo sitta
alisimama na kuwasha kipaza sauti na kusema “waheshimiwa wajumbe katika
mazingira haya tuliyonayo naomba
kutangaza kuwa nasitisha shunguli za
bunge hadi hapo tutakapo tangaziwa tena”
Licha ya kauli hiyo baadhi
ya wajumbe waliendelea kupaza sauti zao
wakisema kwamba walikuwa wanaburuzwa.
Wakati hayo yakitokea
kikoci cha askari wa bunge kiliingilia
ndani ya ukumbi na kusimama katika lango kuu hali iliyoonekana kuwa ni kuchukua tahadhari endapo hali ya usalama ingechafuka.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “DAKIKA TATU ZA WARIOBA MBELE YA MIMBARI YA BUNGE.”
Post a Comment