Tuesday, March 18, 2014
UKAWA WAELEZA SABABU ZA KUMZUIA WARIOBA.
Do you like this story?
Mwenyekiti wa Bunge
maalumu la katiba Samuel sitta alipata jaribuo la kwanza baada ya baadhi ya
wajumbe kupinga kuruhusiwa kwa mwenyekiti
wa tume ya mabadiliko ya katiba jaji Joseph Warioba kuwasilisha rasimu ya katiba kwa madai ya
ukikwaji wa kanuni za bunge.
Wajumbe hao chini ya umoja
wa katiba ya watanzania(ukawa) walitangaza mapema jana kwamba wangepinga ratiba
nzima kuendlea hadi madai yao ya kumtaka Rais Jakaya Kikwete afungue bunge . kwanza kabla ya rasimu
kuwasilishwa yasikilizwe.
Katika uamuzi huo
ulifikiwa jana mchana mmoja wa viongozi wa ukawa profesa ibrahimu lipumba amesema
kwa sababau za ukikwaji wa kanini
tuapenda kueleza kwamba hatupo tayari
kuunga mkono tutapinga kwa kadri uwezo wetu mambo makubwa manne
kufanyika bungeni.
Amesema mambo ambayo
wanapanga ni uwasilishaji wa rasimu ya kativa uliopangwa kufanyika jana kabla
ya ufunguzi wa bunge maalumu unotarajiwa kufanywa na Rais Kikwete.
Profesa lipumba pia
alisema wangepinga kufanyika kwa semina ambyo ilipangwa kuongozwa na wataalamu wa ndani au nje ya nchi leo
kuhusu uzoefu katika masuala ya bunge la katiba.
Pia tutapinga hotuba ya
Rais endapo itatolewa baada ya uwasilishaji
wa rasimu ya katiba na pia jambo jingine lolote linalokiuka kanuni za
bunge maalumu amesema profesa lipumba aliyeambatana na wajumbe wenzake james
mbatia na tundu lissu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “UKAWA WAELEZA SABABU ZA KUMZUIA WARIOBA.”
Post a Comment