Wednesday, April 30, 2014

MTUMBWI WAPINDUKA NA KUUA MWANAFUNZI KYELA.




Watu wawili akiwemo mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika shule ya sekondari Mwigo wilayani Kyela mkoani Mbeya, wanahofiwa kufa maji katika Mto Kiwira.

Hofu ya kufa maji watu hao inakuja baada ya mtumbwi waliokuwa wakiutumia, kupinduka.
Watu hao walikuwa wakitoka kijiji cha Ibungu kwenda kitongoji cha Ndandalo kilichopo Kyela. Mto huo unatajwa kujaa maji, kutokana na mvua nyingi zilizonyesha ukanda wa juu.

Akizungumza na waandishi wa habari juzi baada ya kutokea ajali hiyo,  Mwenyekiti wa kitongoji cha Ndandalo, Lameck Mbembela alisema ajali hiyo ilitokea juzi  saa 10.30 jioni.

Mwenyekiti huyo alisema wakiwa katikati ya mto, mtumbwi uliyumba kutokana na udogo wake, ikilinganishwa na wingi wa maji yaliyokuwa yakitiririka kwa kasi.

0 Responses to “MTUMBWI WAPINDUKA NA KUUA MWANAFUNZI KYELA.”

Post a Comment

More to Read