Sunday, May 18, 2014

WENGER BAADA YA KUBEBA `NDOO` YA FA ASEMA HANG`ATUKI ASERNAL


 Haondoki: Bosi wa Asernal, Aserne Wenger amethibitisha kuendelea kuwepo klabuni hapo

Pati: Lukas Podolski akimlowesha kwa bia bosi wake, mzee  Wenger baada ya kombe la FA

Aogeshwe huyoo: Wenger akiwa amebebwa na kumwagiwa bia na wachezaji wake.

Miaka tisa, Kombe moja: Kocha wa Arsenal, Mfaransa Arsene Wenger alilazimika kubadilisha shati lake baada ya alilokuwa amevaa kuloana bia alizomwagiwa na wachezaji wake wakati wa kushangilia ushindi wa 3-2 uliowapa Kombe la FA jana Uwanja wa Wembley, taji la kwanza kwa klabu hiyo na mocha huyo kwa ujumla baada ya miaka tisa.


Kutoka kushoto ni Santi Carzorla, Mesut Ozil, Per Mertesacker, Serge Gnabry, Lukas Podolski na Aaron Ramsey



KOCHA wa Arsenal, mfaransa,  Arsene Wenger sasa anatarajiwa kusaini mkataba mpya baada ya kufuta ukame wa miaka 9 bila kombe kufuatia kutwaa ndoo ya FA jana kwa kuwanyuka 3-2 Hull City katika mechi ya fainali iliyopigwa dimba la Wembley.

Wenger alisema jambo la kusaini mkataba litafanyika kwasababu yeye na bodi ya timu wapo katika mazingira mazuri.
“Kamwe sijiulizi kuondoka zaidi ya kujiuliza nini klabu yangu ifanye”. Alisema Wenger.

Wenger amekaa Asernal bila kombe kwa siku 3, 283 sawa na miaka 9 na kucheza mechi 512, lakini jana alijifuta machungu pamoja na mashabiki wa Asernal

0 Responses to “WENGER BAADA YA KUBEBA `NDOO` YA FA ASEMA HANG`ATUKI ASERNAL”

Post a Comment

More to Read