Thursday, May 15, 2014
MAUAJI YA ALBINO SIMIYU YAIBUA MAPYA, WADAU WAOMBA SERIKALI IFUTE VIBALI VYA WAGANGA.
Do you like this story?
Shirika la kutetea haki za watu wenye
ulemavu wa ngozi Albino la 'Under the Same Su'n limeiomba serikali kufuta
vibali na shughuli zote za waganga wa jadi kwa madai kuwa wao ndiyo chanzo cha
kuuawa kwao.
Kuuawa kwa mwanamke Munghu Lugata
mlemavu wa ngozi toka kijiji cha Gasuma mkoani Simiyu Kaskazini Magharibi mwa
nchi hiyo kumeacha hisia na uchungu kwa walemavu wengine waliopata mikasa hiyo.
Akizungumza na mwandishi wa BBC Leonrad
Mubali kwa uchungu na kilio, Mariamu Staford mlemavu wa ngozi Albino amesema
kwamba tukio la kuuawa kwa Munghu Lugata mwanamke mwenye umri wa miaka 40 juzi
linamkumbusha mkasa wake uliomkuta wa kukatwa mikono yake yote, zaidi ya miaka
mitano iliyopita na sasa anatumia mikono ya bandia ya vyuma huku akisema
malengo yake mengi yamekwama.
Albino wamekuwa wakihangaishwa sana
nchini Tanzania ambako baadhi ya watu wanaamini kuwa dawa za miujiza
zinazotengezwa kutokana na viungo vya miili yao zinaleta bahati nzuri.
Mashambulizi yamepungua katika siku za
hivi karibuni lakini mauaji ya hivi punde yamepelekea shirika moja la kutetea
haki za Albino kutoa wito kwa serikali kupiga marufuku waganga wote wa
kienyeji.
Matukio mengi ya mauaji ya walemavu
nchini Tanzania yamekuwa yakihusishwa na imani za kishirikina huku waganga wa
jadi wakihusishwa.
Mkoa wa Simiyu ni moja katika maeneo
kaskazini magharibi mwa Tanzania yenye matukio mengi ya mauaji hayo.
Hivi karibuni Tanzania umezinduliwa
mnara maalumu unaoitwa NITHAMINI, mnara pekee duniani unaowakilisha kupinga
mauaji ya albino huku Tanzania ikiwa ni moja ya nchi yenye matukio mengi ya
ukatili dhidi ya walemavu hao
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MAUAJI YA ALBINO SIMIYU YAIBUA MAPYA, WADAU WAOMBA SERIKALI IFUTE VIBALI VYA WAGANGA.”
Post a Comment