Thursday, May 29, 2014
MWENGE WAZUIA MAHABUSU MBEYA.
Do you like this story?
Wakati
Mwenge wa Uhuru ukizua mvutano mkali bungeni, Dodoma kiasi cha Waziri Mkuu
Mizengo Pinda kusimama na kutoa ufafanuzi, ujio wa Mwenge huo wilayani Mbozi
mkoani, Mbeya umesababisha mahabusi waliokuwa wakisubiri kupelekwa mahakamani
jana kukosa gari kwa madai liko kwenye ziara ya Mwenge huo.
Mwendesha
Mashtaka wa Polisi, Joel Mori alisema mahakamani kuwa sababu za kukwama kwa
mahabusi kusomewa mashtaka juzi na jana ni ukosefu wa gari, ambalo kwa sasa
linafanya kazi za Mwenge.
Aliiomba
mahakama kupanga tarehe nyingine ya kusikiliza kesi na Hakimu Nemes Chami,
alisema kesi hizo zitasikilizwa Juni 9, mwaka huu.
Katika
kipindi cha maswali na majibu juzi wabunge wa upinzani walisimama wote kupinga
mbio za Mwenge kwa madai hazina tija. Juzi, Pinda alitoa ufafanuzi kuwa hakuna
dhambi kwa Mwenge kuendelea kukimbizwa nchini kwa kuwa unaimarisha uzalendo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MWENGE WAZUIA MAHABUSU MBEYA.”
Post a Comment