Saturday, May 31, 2014
PIGO TENA BONGO MUVI: GEORGE TYSON AFARIKI DUNIA.
Do you like this story?
NI pigo tena
kwa tasnia ya Bongo Muvi, mwongozi filamu Bongo na aliyekuwa mume wa staa wa
filamu za Kibongo, Yvonny Cherry 'Monalisa', George Tyson amefariki dunia baada
ya kupata ajali mbaya ya gari maeneo ya Gairo, Morogoro akitokea mkoani Dodoma.
Tyson
alikuwa ameambatana na watu kadhaa katika safari hiyo ambao wanadaiwa kuumia
vibaya. Mwili wa marehemu Tyson pamoja na majeruhi wa ajali hiyo wamepelekwa
Hospitali ya Mkoa wa Morogoro. Tyson enzi za penzi lake na Monalisa
walifanikiwa kupata mtoto aitwaye Sonia.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “PIGO TENA BONGO MUVI: GEORGE TYSON AFARIKI DUNIA.”
Post a Comment