Tuesday, June 3, 2014

HATIMAYE MTOTO NASRA ALIYEFUNGIWA NDANI YA BOKSI AZIKWA LEO MJINI MOROGORO





Mfanyabiashara, Al Saed Omary aliyefanikisha kuleta mwili wa marehemu Nasra kutoka Dar es Salaam.


 Mbunge Abdulaziz Abood akiweka udongo katika kaburi la marehemu Nasra na kuahidi kumfanyia hitma baada ya siku 40 tangu kuzikwa kwake.

 Hatimaye Mtoto Nasra Mvungi aliyefariki Juni mosi mwaka huu kufuatia kuishi katika mateso makubwa kutoka kwa mama yake mkubwa baada ya mama yake kufariki na kuishi katika boksi bila huduma muhimu anazostahili kupatiwa binadamu hasa mtoto mdogo mwenye umri wa mwaka mmoja amezikwa kwa heshima zote na wakazi wa Morogoro wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo, Joel Nkaya Bendera, Mbunge wa Morogoro mjini, Abdulaziz Abood na mfanyabiashara wa mabasi na vituo vya mafuta mkoani Morogoro Al Saed Omary. 

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, ametaka vyombo vya sheria Mahaka, kutoa hukumu inayowastahili waliohusika kwa mateso na kupelekea kifo cha Nasra.

0 Responses to “HATIMAYE MTOTO NASRA ALIYEFUNGIWA NDANI YA BOKSI AZIKWA LEO MJINI MOROGORO ”

Post a Comment

More to Read