Sunday, June 1, 2014
MIZENGO PINDA ATAKA KANUNI ZA BUNGE ZIBADILISHWE.
Do you like this story?
Uamuzi
wa wabunge wa Kambi Rasmi ya Upinzani kutoka nje ya Ukumbi wa Bunge wakisusia
uhitimishaji wa mjadala wa Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini,
kimemzindua Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ambaye amependekeza kubadilishwa kwa
kanuni za Bunge ili kuwadhibiti.
Pinda
alitoa kauli hiyo juzi usiku baada ya bajeti hiyo iliyogomewa na wapinzani
kupitishwa na wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) pekee, huku akisisitiza kuwa
tabia hiyo ifike wakati ikomeshwe.
Wabunge
hao wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), waliamua kususia mjadala huo
kwa madai ya kutoridhishwa na ulivyokuwa ukiendeshwa kwa mikakati waliyowekeana
wabunge wa CCM ya kufukia kashfa nzito ya IPTL inayoikabili wizara hiyo.
Kiongozi
wa Kambi hiyo, Freeman Mbowe amesema amefuatilia mjadala huo, lakini kwa bahati
mbaya umegubikwa na ukinzani wa kiitikadi na makundi, kwamba wabunge wanajadili
kwa kujaribu kufukia mambo mazito kwa sababu ya mitazamo ya makundi na kiitikadi,
hivyo siyo busara kuendelea kushiriki
.
Katika
maelezo yake, Pinda amesema: “Inawezekana kanuni zinaruhusu, lakini haiwezekani
kila mnaposhindwa hoja muone njia rahisi ni kutoka nje, nasema hivi ili
Watanzania waone kuwa hali hii siyo nzuri.
”
Amesema
hoja zikitolewa wapinzani wanatakiwa kukaa na kuzisikiliza na kwamba jibu siyo
kutoka nje bali ni kushindana hadi hatua ya mwisho.
“Tabia
inaendelea kujengeka na siyo nzuri. Tuombe kanuni za Bunge zirekebishwe kwa
sababu Bunge linaonekana halina watu wakati hao waliotoka hawana sababu za
msingi” alisema Pinda.
Pinda
aliiponda taarifa ya upinzani iliyosomwa na Waziri Kivuli wa Nishati na Madini,
John Mnyika kwamba haikuwa na jambo la msingi na ilijaa maneno mengi.
Akizungumzia
sakata la IPTL, Pinda alisema jambo hilo sasa linachunguzwa na Mdhibiti na
Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) pamoja na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na
Rushwa (Takukuru), kuwataka wabunge kutolijadili mpaka hapo ukweli utakapowekwa
wazi.
Pinda
amesema ili kuhakikisha huduma za umeme na maji zinawafikia wananchi,
amemwagiza Waziri wa Fedha kufumba macho kutafuta fedha ikibidi hata kukata
fedha za posho ili ziende katika miradi ya maji na umeme.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MIZENGO PINDA ATAKA KANUNI ZA BUNGE ZIBADILISHWE.”
Post a Comment