Sunday, June 1, 2014
KASHFA SABA NZITO NCHINI.
Do you like this story?
Serikali
imepoteza zaidi ya Sh362.9 bilioni kutokana na baadhi ya kashfa kubwa za
ufisadi na operesheni mbalimbali zilizoligharimu taifa tangu uhuru.
Uchunguzi
umebaini taifa kubwa na kashfa mbalimbali za upotevu wa fedha au kuanzisha
mipango ambayo utekelezaji wake ulisababisha maumivu kwa wananchi na hakuna
awamu ya uongozi wa Serikali iliyokwepa hali hiyo.
Kuanzia
awamu ya kwanza ya Mwalimu Julius Nyerere aliyeiongoza nchi toka mwaka 1961
ilipopata uhuru hadi 1986, Rais Ali Hassan Mwinyi (1986-1995), Rais Benjamin
Mkapa (1995-2005) na Rais Jakaya Kikwete (2005-hadi sasa), kumeibuka kashfa
mbalimbali, saba zikiwa kubwa na kulitikisa taifa.
Kashfa
na operesheni saba kubwa zilizotikisa taifa ni pamoja na Operesheni Uhujumu
Uchumi, ufisadi katika Mfuko wa Kuwezesha Uagizaji Bidhaa kutoka Nje ya Nchi
(Commodity Import Support – CIS) na Kashfa ya Rada.
Nyingine
ni ufisadi Akaunti ya EPA, kashfa ya Richmond, Operesheni Tokomeza Ujangili na
ile ya uchotaji mabilioni katika akaunti ya Escrow.
Mwaka
1984 Serikali ilianzisha Operesheni Uhujumu Uchumi, iliyoongozwa na Waziri Mkuu
wa wakati huo, Edward Sokoine ili kutaifisha mali ambazo baadhi ya watu
walidaiwa kujipatia kwa njia isiyo halali.
Operesheni
hiyo ilishuhudia baadhi ya watuhumiwa wakimwaga fedha mitaani na majalalani,
huku wengine wakitupa mali kuhofia kutiwa kwenye mkono wa sheria.
Hata
hivyo, katika operesheni hiyo baadhi ya watendaji wa Serikali ambao hawakuwa
waaminifu, waliitumia nafasi hiyo vibaya kutaifisha mali za baadhi ya watu,
ambao hawakuwa wahujumu uchumi.
Zoezi
hilo lilisababisha wananchi kadhaa hasa vijijini kuwekwa ndani na wengine
kuachwa maskini baada ya kunyang’anywa mali zao ikiwamo mifugo na mashine za
kusaga nafaka, kwa kudaiwa kuwa walizipata kwa njia isiyo halali.
Miaka
24 baadaye yaani mwaka 2008, liliibuka sakata jingine lililokuwa na harufu
kubwa ya ufisadi wa mabilioni katika Mfuko wa Kuwezesha Uagizaji Bidhaa kutoka
Nje ya Nchi (Commodity Import Support – CIS).
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “KASHFA SABA NZITO NCHINI.”
Post a Comment