Tuesday, June 3, 2014
SERIKALI IMEKIRI KASI YA KUPAMBANA NA VITENDO VYA UDHALILISHAJI KWA WANAWAKE KWENYE KUMBI ZA STAREHE NI NDOGO.
Do you like this story?
Serikali imekiri kuwa kasi ya kupambana
na vitendo vya udhalilishaji wanavyofanyiwa wanawake kwenye baadhi ya kumbi za
starehe hapa nchini ni ndogo
Kauli hiyo imetolewa bungeni Dodoma hii
leo na naibu waziri wa habari, vijana utamaduni na michezo Mh Juma Nkamia
wakati wa kipindi cha maswali na majibu
Mh. Nkamia amesema kumekuwepo na
vitendo vya udhalilishaji na aibu wanavyofanyiwa wanawake katika kumbi hizo
ikiwemo kucheza nusu utupu ama wakati mwingine kucheza utupu na vitendo vingine
ambavyo ni kinyume na sheria na taratibu za nchi
Amesema tayari hatua
zimekwishachukuliwa na serikali ikiwemo kuyafungia mashindano ya miss utalii,
na vikundi vya "kanga moko" ambavyo vimebainika kuongoza kwa
udhalilishaji na kusema kuwa serikali haitaishia hapo bado itazidi kuchukua
hatua kwa vikundi vitakavyokiuka ingawa amekiri kuwa serikali inafanya hivyo
polepole
"Serikali makini ni ile inayofanya
kazi zake taratibu na kwa umakini, wanasema harakaharaka haina baraka"
amesema Nkamia
Vitendo hivi vimeonekana kushamiri kwa
baadhi ya kumbi za starehe ambapo wanawake hao hufanya hivyo kwa madai ya
kuahidiwa donge nono na wengine wamekuwa wakidhulumiwa mara baada ya kufanyiwa
vitendo hivyo vya aibu
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “SERIKALI IMEKIRI KASI YA KUPAMBANA NA VITENDO VYA UDHALILISHAJI KWA WANAWAKE KWENYE KUMBI ZA STAREHE NI NDOGO.”
Post a Comment