Tuesday, June 3, 2014
TAIFA STARS BAADA YA KUITUNGUA ZIMBABWE, SASA YAANZA MAWINDO YA KUWANG`OA MSUMBIJI.
Do you like this story?
Timu ya taifa ya soka Tanzania Taifa Stars, chini ya
kocha Mholanzi, Mart Nooij, inatarajia kuingia kambini Jumatano ijayo kwa ajili
ya kujiwinda na mchezo dhidi ya Msumbiji kuwania kupangwa hatua ya
makundi ili kusaka tiketi ya fainali za AFCON zitakazochezwa Morocco hapo
mwakani.
Taifa Stars imewasili kutokea Harare ambako
ilifanikiwa kufuzu hatua inayofuata baada ya kuingoa Zimbabwe kwa jumla
ya magoli 3 - 2.
Stars ilishinda bao 1-0 katika mchezo wa kwanza
jijini Dar es salaam na kufanikiwa kutoka sare ya 2-2 mjini Harare, mwishoni
mwa wiki iliyopita.
Shujaa wa Tanzania katika mchezo huo wa marudiano
walikuwa ni nahodha Nadir Haroub `Canavaro` na mshambuliaji wa kimataifa wa
Tanzania, Thomas Ulimwengu.
Afisa habari wa Shirikisho la mpira wa miguu
Tanzania TFF, Boniface Wambura Mgoyo amesema timu hiyo inataraji kuingia
kambini kwa mara nyingine kujiwinda dhidi ya Msumbiji Jumatano ijayo kwasababu
mwalimu anatakiwa kupata muda wa kutosha kufanyia marekebisho makosa
yaliyojitokeza mechi zilizopita.
Taifa Stars inataraji kucheza dhidi ya
Msumbiji hapo Julai 19 na 20 mwaka huu sanjari na timu nyingine za ukanda wa
CECAFA Kenya, Uganda na Rwanda ambazo zimepenya hatua inayofuata.
Wakati huo huo, mtandao huu umekutana na John Jambele
ambaye ni miongoni mwa wadau ambao wanaonesha kufurahishwa na matokeo
bora ya Taifa Stars ambapo anawataka wachezaji hao kukaza uzi zaidi na
kutobweteka kwa hatua waliyofikia.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “TAIFA STARS BAADA YA KUITUNGUA ZIMBABWE, SASA YAANZA MAWINDO YA KUWANG`OA MSUMBIJI.”
Post a Comment