Thursday, October 16, 2014
MPIGA DEBE HUYU AUSHANGAZA UMMA MKOANI MBEYA KWA KITENDO ALICHOFANYA
Do you like this story?
Katika hali isiyokuwa
ya kawaida, mpigadebe maarufu katika kituo cha mabasi cha mbalizi wilayani mbeya
amenunua mbuzi wawili na bidhaa nyingine za aina mbalimbali zenye thamani ya
zaidi ya shilingi milioni moja na kuzipeleka kwenye vituo vya watoto yatima
kama zawadi huku akiwaasa watoto hao kutoshawishika kwenda kupiga debe kwenye
vituo vya mabasi.
Mpigadebe maarufu
katika kituo cha mabasi cha mbalizi, Anganile Mwamuluma Andrea ambaye amefanya
kazi hiyo kwa zaidi ya miaka 20 ameushangaza umma wa wakazi wa mbeya baada ya
kuamua kununua mbuzi wawili, mchele, maharagwe, sabuni, mafuta ya kupikia na mahindi
na kupeleka bidhaa hizo katika vituo viwili vya watoto yatima ambako amezitoa
kama zawadi kwa watoto hao, huku akiwaasa kutoshawishika kujihusisha na kazi ya
kupiga Debe kwenye vituo vya mabasi.
Walimu wa watoto hao
wameeleza kushtushwa na kitendo cha mpigadebe huyo, lakini wakasema kuwa ni
mfano Bora wa kuigwa kwa vijana wanaofanikiwa kukumbuka mazingira walikotoka,
huku wakiwahimiza wazazi kuongeza upendo kwa watoto wao ili kupunguza wimbi la
watoto wanaoishi katika mazingira magumu nchini.
Baadhi ya watoto
ambao wamepokea msaada huo, wamemshukuru mpigadebe huyo na kuwataka watu
wengine kupata funzo la kuthamini na kuwapenda watoto ikiwa ni pamoja na
kuwaandalia mazingira mazuri ya kujitegemea.
ITV
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MPIGA DEBE HUYU AUSHANGAZA UMMA MKOANI MBEYA KWA KITENDO ALICHOFANYA ”
Post a Comment