Saturday, October 11, 2014
NEC: HAKUNA KURA YA MAONI BILA DAFTARI JIPYA
Do you like this story?
Dar es Salaam. Tume
ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema haitaendesha uchaguzi wa aina yoyote, wala
kuitisha kura ya maoni hadi kazi ya kuboresha daftari la kudumu la wapiga kura
itakapokamilika.
Kauli ya NEC imekuja
siku moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kukabidhiwa Katiba inayopendekezwa na
Mwenyekiti wa lililokuwa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta na kulitaja
suala la uboreshaji wa daftari la hilo kama mambo matatu yanayoiweka kura ya
maoni kupitisha Katiba hiyo njiapanda.
Mambo mengine ni
Sheria inayotaka kura hiyo ipigwe ndani ya siku 84 baada ya Katiba
inayopendekezwa kuchapishwa na kufanyiwa marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya
Katiba.
Mwenyekiti wa NEC,
Jaji Damian Lubuva alisema jana kwamba kuendesha uchaguzi bila kuboresha
daftari hilo ni kuongeza malalamiko kwa wananchi na wadau, hususan vyama vya
siasa.
“Msimamo wetu (NEC)
ni kuwa bila daftari kuboreshwa hatuko tayari kuendesha uchaguzi wowote na hata
huo wa kura ya maoni,” alisema na kuongeza:
“Sasa tuna takriban
vijana milioni 2.3 ambao wamefikisha umri wa kupiga kura ... lakini kuna watu
waliokufa, vyote hivi vinatakiwa kuboreshwa kwanza na sisi Tume hatuko tayari,
naomba muwaambie wananchi.”
Kuhusu hoja kwamba NEC
itumie daftari lililopo kama ambavyo wamekuwa wakifanya katika uchaguzi mdogo
mara kwa mara pale mbunge anapofariki dunia, Jaji Lubuva alisema tume yake
haitaki yajirudie malalamiko ambayo imeyapata kupitia uchaguzi wa aina hiyo.
“Katika Uchaguzi wa
Kalenga, Arumeru Mashariki na Chalinze, tulilalamikiwa sana kuhusu matumizi ya
daftari hili, hivyo kutokana na malalamiko hayo yaliyotoka kwa vyama vya siasa,
hatutaki tena kupata mengine kama hayo, ndiyo maana nasema muwaambie wananchi
kwamba hatutaendesha chaguzi zozote hadi pale tutakapoboresha daftari,” alisema
Jaji Lubuva.
Kuhusu lini kazi ya
kuboresha daftari hilo itaanza, Jaji Lubuva alisema: “Tunasubiri vifaa vifike
na vitakapofika tu tutaanza mara moja.”
Kauli ya Rais Kikwete
Akizungumza juzi
katika sherehe ya makabidhiano ya Katiba inayopendekezwa kwenye Uwanja wa
Jamhuri mjini Dodoma, Rais Kikwete alielezea maeneo matatu yenye utata ambayo
yanatakiwa kupatiwa ufumbuzi ili kufanikisha hatua hiyo.
Alisema suala la
kwanza ni ratiba iliyotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuelekea Uchaguzi
Mkuu ujao ambayo inaonyesha mchakato wa kuandika upya Daftari la Wapiga Kura
utakamilika Mei 2015. (MWANANCHI)
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ NEC: HAKUNA KURA YA MAONI BILA DAFTARI JIPYA ”
Post a Comment