Saturday, October 11, 2014
MAOFISA POLISI 120 WATIMULIWA CCP
Do you like this story?
Moshi. Maofisa wa Polisi wapatao 120 wa
Jeshi la Polisi, waliokuwa wakihudhuria mafunzo ya kupandishwa vyeo katika Chuo
cha Taaluma ya Polisi Moshi (MPA), wametimuliwa chuoni hapo.
Vyanzo mbalimbali
vililidokeza kuwa, waliotimuliwa chuoni hapo ni maofisa ambao wana
ulemavu wa aina mbalimbali walioupata wakiwa wanatekeleza majukumu yao ya kazi.
Habari hizo zilisema
hadi jana saa 9:00 alasiri, maofisa hao walikuwa ofisi za mkuu wa chuo hicho
wakisubiri kupatiwa maelekezo ya namna ya kurejea katika vituo vyao vya kazi
mikoa mbalimbali.
“Wako 120 hivi
walikuja hapa (MPA) kwa ajili ya kuchukua kozi za Koplo, Sajenti, Meja na
‘Assistant Inspector’ (wakaguzi wasaidizi), lakini ndiyo hivyo wametuambia
tuondoke,” kilidokeza chanzo chetu.
Hata hivyo, ofisa
mmoja alilidokeza kwamba mkuu wa zamani Jeshi la Polisi (IGP), Said
Mwema, ambaye amestaafu, ndiye wa kulaumiwa kwa kutoheshimu mapendekezo ya
wataalamu.
“Tulimwambia IGP
Mwema kwamba ni vizuri kama maofisa wenye ulemavu kama baadhi ya vigezo wanavyo
basi wapewe vyeo huko huko mikoani, lakini wasiende chuoni,” alidokeza na
kuongeza;
“Tulipendekeza
yafunguliwe madarasa ya kanda wakishafanya mtihani wa kawaida wapewe vyeo huko
huko, lakini wakija chuoni ni lazima wahudhurie vipindi vyote ambavyo vinafanya
chuo kiitwe chuo.
“Chuo chochote kile
kina vigezo vyake na kwamba ili mtu apate cheo alichokwenda kukisomea ni lazima
ahudhurie asimilia 95 ya vipindi ikiwamo kwata, medani za kivita na kuzuia
vurugu,”amesema.
Chanzo kingine
kililidokeza kuwa maofisa hao waliripoti chuoni hapo wiki mbili
zilizopita na katika uchunguzi, walibainika wana ulemavu ambao hawawezi kumudu
mafunzo ya ukakamavu.
Mmoja wa maofisa hao
waliotimuliwa alilalamika kuwa kitendo hicho siyo cha kiungwana kwa kuwa ulemavu
huo waliupata wakiwa kazini wakilitumikia Taifa na hawajashindwa kuingia
darasani.
“Baadhi yetu
tumefanya kazi miaka 20 wengine 25. Wamekatika miguu. Wako trafiki wamegongwa
na polisi wengine wamepigwa risasi na majambazi wakapata ulemavu si sawa kutunyima
vyeo,” alidai. (MWANANCHI)
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ MAOFISA POLISI 120 WATIMULIWA CCP”
Post a Comment