Friday, January 23, 2015

KIJANA ANGANDISHWA KWA ZAIDI YA MASAA 7 MARA BAADA YA KUIBA SIMU.MBEYA


kijana Ommary Said (20) Mkazi wa Sokomatola jijini mbeya akiwa amekachini huku akiwa ameshika fimbo ya mganga wa huyo  mara baada ya kukwapua simu na kugandishwa kwa zaidi ya masaa 7 eneo la stendi kuu ya mabasi jijini Mbeya
Kijana huyo ambaye ni teja akisimulia kilicho mkuta mara baada ya kukwapua simu ya mama huyo ambapo aligandishwa kwa zaidi ya masaa 7.
Fimbo aliyoshika ndiyo iliyomsaidia kumpa nguvu  ya kutembea ambayo nayo ilitoewa na mama huyo kama sehemu ya kinga na ngao anayotumia mganga huyo katika shughuli zake za kitaabibu
Mganga huyo Chiku Ramadhan kutoka Mkoani Tabora akiwa moja ya ofisi za kukatia tiketi katika kituo cha mabasi Mbeya kwa lengo la kupiga lamri mara baada ya kuombwa na wahusika wa ofisi hiyo ili kukamata wezi.
Kijana Ommary baada ya kuachiwa huru na mganga huyo
Mganga huyo mwenye koti akitoa masharti kwa mtuhumiwa wake .
Picha na David Nyembe wa Fahari News


Na Mwandishi wetu,Mbeya
Katika hali isiyokuwa ya kawaida kijana mmoja aliyefahamika kwa jina Ommary Said (20) Mkazi wa Sokomatola jijini mbeya amejikuta katika wakati mgumu mara baada ya kudaiwa kukwapua simu ya mmoja wa abiria katika kituo hicho cha mabasi jijini hapa na kugandishwa kwa zaidi ya masa7.

Tukio hilo la aina  yake limetokea leo jijini hapa ambapo inadaiwa kuwa kijana huyo katika harakati zake za kutafuta abiria aliingia anga  mbaya ambapo alikwapua simu ya mmoja wa abiria na kutokomea nayo ambapo muda mchache mara baada ya kukwapua simu hiyo alipiga hatua chache kisha kuganda hali ambayo iliibua mshangao kwa watu waliopo katika eneo hilo la stendi kuu ya mabasi jijini hapa.

Inadaiwa kuwa kijana huyo  Omary Saidi (20) mkazi wa Sokomatola ambaye pia ni mtumiaji wa dawa za kulevya(Teja)  mara baada ya kuchukua simu hiyo alihisi hali tofauti ambapo alirudi na kumkabidhi mtu huyo alijitambulisha kwa jina  Chiku Ramadhani kutoka Tabora ambaye anadaiwa kuwa ni mganga wa kienyeji   huku akitoa sauti ya huruma kwakuomba asamehewe kwa kitendo hicho.


Akizungumzia tukio  Mganga huyo Chiku Ramadhani, amesema aliwasili Jijini Mbeya jana January 21 akitokea Jijini Dar es Salaam, akiwa katika eneo la stendi kuu, aliingia kwenye moja ya mgahawa kwa ajili ya kupata chakula, alipomaliza alienda kunawa mikono huku simu yake akiwa ameicha kwenye meza aliyokuwa akiitumia.

0 Responses to “KIJANA ANGANDISHWA KWA ZAIDI YA MASAA 7 MARA BAADA YA KUIBA SIMU.MBEYA”

Post a Comment

More to Read