Friday, January 23, 2015
KIJANA ANGANDISHWA KWA ZAIDI YA MASAA 7 MARA BAADA YA KUIBA SIMU.MBEYA
Do you like this story?
Kijana huyo ambaye ni teja akisimulia kilicho mkuta mara baada ya kukwapua simu ya mama huyo ambapo aligandishwa kwa zaidi ya masaa 7. |
Fimbo aliyoshika ndiyo iliyomsaidia kumpa nguvu ya kutembea ambayo nayo ilitoewa na mama huyo kama sehemu ya kinga na ngao anayotumia mganga huyo katika shughuli zake za kitaabibu |
Kijana Ommary baada ya kuachiwa huru na mganga huyo |
Mganga huyo mwenye koti akitoa masharti kwa mtuhumiwa wake . |
Picha na David Nyembe wa Fahari News |
Na Mwandishi wetu,Mbeya
Katika hali isiyokuwa ya kawaida kijana mmoja aliyefahamika kwa
jina Ommary Said (20) Mkazi wa Sokomatola jijini mbeya amejikuta katika wakati
mgumu mara baada ya kudaiwa kukwapua simu ya mmoja wa abiria katika kituo hicho
cha mabasi jijini hapa na kugandishwa kwa zaidi ya masa7.
Tukio hilo la aina yake limetokea leo jijini hapa ambapo
inadaiwa kuwa kijana huyo katika harakati zake za kutafuta abiria aliingia
anga mbaya ambapo alikwapua simu ya
mmoja wa abiria na kutokomea nayo ambapo muda mchache mara baada ya kukwapua
simu hiyo alipiga hatua chache kisha kuganda hali ambayo iliibua mshangao kwa
watu waliopo katika eneo hilo la stendi kuu ya mabasi jijini hapa.
Inadaiwa kuwa kijana huyo Omary Saidi (20) mkazi wa Sokomatola ambaye
pia ni mtumiaji wa dawa za kulevya(Teja) mara baada ya kuchukua simu hiyo alihisi hali
tofauti ambapo alirudi na kumkabidhi mtu huyo alijitambulisha kwa jina Chiku Ramadhani kutoka Tabora ambaye anadaiwa
kuwa ni mganga wa kienyeji huku akitoa sauti ya huruma kwakuomba asamehewe
kwa kitendo hicho.
Akizungumzia tukio Mganga
huyo Chiku Ramadhani, amesema aliwasili Jijini Mbeya jana January 21 akitokea
Jijini Dar es Salaam, akiwa katika eneo la stendi kuu, aliingia kwenye moja ya
mgahawa kwa ajili ya kupata chakula, alipomaliza alienda kunawa mikono huku
simu yake akiwa ameicha kwenye meza aliyokuwa akiitumia.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “KIJANA ANGANDISHWA KWA ZAIDI YA MASAA 7 MARA BAADA YA KUIBA SIMU.MBEYA”
Post a Comment