Thursday, January 29, 2015
MGANGA WA DIAMOND JELA MIAKA 7.
Do you like this story?
![]() |
Msanii Diamond |
Yule mganga
aliyejitapa kumtengenezea nyota ya mvuto staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul
‘Diamond Platnumz’, Ustadh Yahya amehukumiwa kifungo cha miaka saba (7) jela
baada ya kukutwa na hatia katika kisa cha kuchanganya akihusishwa na wizi wa
gari.
Habari za
uhakika zilieleza kwamba aliyehitimisha kesi hiyo ni Hakimu Mkazi Mwandamizi wa
Mahakama ya Wilaya ya Ilala jijini Dar, Hassan Kisailo mapema Jumatatu wiki hii
wakati jua la asubuhi likiwaka.
Huku kijasho
chembamba kikimtiririka huku akishusha miwani kidogo kuona wahudhuriaji wa kesi
hiyo, Hakimu Kisailo alitoa hukumu hiyo kwa maelezo kwamba, mnamo Januari 20,
mwaka jana, maeneo ya Kariakoo jijini Dar, Yahya alidaiwa kuiba gari aina ya
Toyota RAV4 lenye namba za usajili T 139 BSJ likiwa na thamani ya Sh. milioni
12, mali ya Edrick Elieza.
Wakati Hakimu
Kisailo akisoma hukumu hiyo, mshtakiwa na wadhamini wake hawakuwepo mahakamani
hapo hivyo alisema mara tu baada ya hukumu wahusika hao watakamatwa ili
wakatumikie adhabu inayowakabili.
Huku akiangalia kulia na kushoto, Hakimu Kisailo
alisema kuwa, baada ya kuupitia mtiririko wa kesi hiyo, alibaini kwamba ni
kweli mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo hivyo alimhukumu kwenda jela miaka 7.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MGANGA WA DIAMOND JELA MIAKA 7.”
Post a Comment