Wednesday, December 16, 2015

PAUL NONGA ATUA YANGA RASMI KWA MKATABA WA MIAKA MIWILI




Rasmi Yanga imekibomoa kikosi cha Mwadui FC baada ya kumnasa mshambuliaji wake, Paul Nonga.

Nonga amejiunga na Yanga kwa mkataba wa miaka miwili, leo.

Awali Nonga alisafirishwa na Yanga kutoa Mwadui, Shinyanga kwa ajili ya kumalizia mazungumzo na mambo yamekamilika leo.

Kabla ya kujiunga na Mwadui FC, Nonga alikuwa mmoja wa washambuliaji hatari wa Mbeya City chini ya Juma Mwambusi ambaye sasa ni kocha msaidizi wa Yanga na inaelezwa ndiye aliyempendekeza.

0 Responses to “PAUL NONGA ATUA YANGA RASMI KWA MKATABA WA MIAKA MIWILI”

Post a Comment

More to Read