Friday, December 25, 2015

WATOTO 23 WAZALIWA KWENYE SIKUKUU YA CHRISMASI MBEYA


Mwanaidi Alphani mkazi wa Ilomba akiwa amemshika mtoto wake wa kiume  kwa furaha(Picha na David Nyembe wa Fahari News)

Mwenekano wa lango kuu la kuingilia Hospitali ya Wazazi Meta(Picha na David Nyembe wa Fahari News)







NA SAMWEL NDONI, MBEYA
JUMLA ya watoto 23, wamezaliwa usiku wa kuamkia  mkesha wa krisimasi katika hospitali ya kanda ya  rufaa Mbeya kitengo cha huduma ya wazazi na mtoto  Meta.

Muuguzi wa zamu wa hospitali hiyo Fatuma Mkinga alisema kuwa kati ya watoto hao wakiume ni 13 na wa kike ni 10 na kwamba hali zao zinaendelea vizuri.

Mkinga amesema kuwa kati yao watoto 12, walizaliwa kwa njia ya kawaida na 11, walizaliwa kwa njia ya upasuaji na wazazi wao wamelazwa katika hospitali hiyo wakiwa chini ya uangalizi.

“Tangu usiku wa kuamkia leo (jana), mpaka muda huu jumla ya watoto 23, wamezaliwa kati yao wakiume ni 13 na wakike ni 10 wote hali zao ni nzuri, pia wapo waliozaliwa kwa njia ya oporesheni” alisema.

Baadhi ya wanawake waliojifungua hospitalini hapo wamesema kuwa wanajisikia vizuri kujifungua siku aliyozaliwa yesu huku wakielezea kuridhishwa na huduma waliyopatiwa na madaktari pamoja na wauguzi wa hospitali hiyo.

“Najisikia vizuri kujifungua mtoto wangu wa kwanza wa kiume siku ya leo (jana), nimejifungua salama kwa njia ya kawaida namshukuru Mungu kwa hilo” alisema Mwanaidi Alphani mkazi wa Ilomba jijini hapa.

Naye Tumpe Nyalile, mkazi wa Nzovwe aliyejifungua kwa njia ya oparesheni amesema kuwa  anaridhishwa na huduma aliyoipata kutoka kwa wahudumu wa hospitali hiyo kuanzia hatua ya mwanzo.

“Najisikia vizuri kujifungua siku ya leo, nawashukuru madaktari na manesi kwa huduma nzuri waliyonipatia, nimejifungua mtoto wa kike nitampatia jina la mariamu,jina la mama yake yesu ambaye naye tunaamini alijifungua siku kama ya leo”amesema

MWISHO



0 Responses to “WATOTO 23 WAZALIWA KWENYE SIKUKUU YA CHRISMASI MBEYA”

Post a Comment

More to Read