Thursday, August 25, 2016

UTEUZI MPYA WA RAIS MAGUFULI






Leo tarehe 25, Agosti 2016 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli amemteua Andrew Willosn Massawe kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu mpya wa Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa “NIDA”.

Kabla ya uteuzi wa leo Andrew Massawe alikuwa Mkurugenzi wa Mifumo ya Kompyuta BOT.

Bw. Massawe anachukua nafasi ya Dkt. Modestus Kipilimba ambaye ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa.

Uteuzi wa Bw. Massawe utaanza mara moja.

0 Responses to “UTEUZI MPYA WA RAIS MAGUFULI ”

Post a Comment

More to Read