Saturday, August 13, 2016
YANGA YAPATA USHINDI WA KWANZA BAADA YA MIAKA 18.
Do you like this story?
Hatimaye
wawakilishi pekee wa Tanzania katika michuano ya kombe la Shirikisho Afrika
(Confederation Cup) klabu ya Yanga leo imepata ushindi wa kwanza katika
michuano hiyo baada ya kufanikiwa kuifunga timu ya MO Bejaia kwa goli 1-0 na
kuibuka na pointi tatu.
Goli
pekee kwenye mchezo huo limefungwa na Amis Tambwe dakika ya nne akimalizia
mpira uliotemwa na golikipa wa Bejaia Chamseddine Rahmani aliyeokoa mpira wa
kichwa wa Simon Msuva.
Ushindi
huo ni wa kwanza kwa Yanga katika hatua hiyo katika miaka ya hivi karibuni,
ikumbukwe mwaka 1998 mabingwa hao wa Tanzania walifika hatua ya makundi katika
michuano ya Klabu Bingwa Afrika lakini hawakufanikiwa kushinda mechi hata moja
badala yake waliambulia sare mbili.
Matokeo
ya leo yanafufua tena matumaini ya Yanga kusonga mbele lakini wakati huo
ikitegemea pia matokeo ya timu nyingine. Ili Yanga ifuzu kucheza hatua ya nusu
fainali, inatakiwa kushinda mechi yake ya mwisho ugenini dhidi ya TP Mazembe
lakili ikiomba Mazembe iifunge Medeama kisha mchezo utakaozikutanisha MO Bejaia
dhidi ya Medeama umalizike kwa sare.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “YANGA YAPATA USHINDI WA KWANZA BAADA YA MIAKA 18.”
Post a Comment