Tuesday, April 18, 2017
Mtuhumiwa aruka kwenye gari la polisi na kukimbia wakati akipelekwa mahakamani
Do you like this story?
Mtuhumiwa
Mohammed Mwalim Ali mkaazi wa Pujini kisiwani Pemba anaekabiliwa na
shitaka la wizi na unyang’anyi ametoroka na kukimbia kusikojulikana
wakati akipelekwa mahakamani akiwa chini ya uangalizi wa Polisi.
Mtuhumiwa
huyo alichupa katika gari ya polisi wakati iliposimama nje ya mahakama
ya Mkoa Chake Chake alipofikishwa leo asubuhi kwa ajili ya kwenda kujibu
kesi hiyo inayomkabili.
Mtuhumiwa
huyo na wenzake watano wanatuhumiwa kufanya wizi wa fedha riali 250
sawa na milioni mbili za kitanzania pamoja na vito mbali mbali vya
mapambo ikiwemo mikufu, pete na vitu vyengine vyenye thamani ya zaidi
ya shilingi milioni 3, mali ya Moza Hilal Shamis mkaazi Kichaka Mtangani
Mkoani Pemba .
Imedaiwa
mahakamani hapo Mtuhumiwa Mohammed Mwalim Ali, na wenzake Saleh Juma
Muhene , Othaman Awesu Bakar, Khalfan Mwalim Khalfan(Fangasi, Khamis
Juma Hemed, kinyume cha Sheria walitenda kosa la uvamizi na kuiba, huku
Bi Mgeni Amour Kombo (32) akituhumiwa kupokea mali za wizi.
Hakim
wa Mahakama ya Mkoa Chake Chake Khamis Ali Simai ameagiza kutafutwa na
kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo na kufikishwa mbele ya mahakama hiyo, huku
washitakiwa namba 3 na 4 Othman Awesu Bakar na Khalfan Mwalim Khalfan
wakirejeshwa rumande hadi April 27 mwaka huu, wengi watatu wamepatiwa
dhamana.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)