Tuesday, April 18, 2017

Muumini akamatwa akiiba sadaka kanisani


Muumini mmmoja wa Kanisa la EAGT Jerusalem Kata ya Majengo, Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga amekamatwa na waumini wenzake kwa madai ya kuiba sadaka wakati wakiwa katika maombi.
Tukio hilo lilitokea Jumapili iliyopita Aprili 9 saa 11 jioni wakati Mchungaji Felix Gwamiye, akiongoza maombi huku waumini wakiwa wamefumba macho na mtuhumiwa huyo alijifanya anatoa sadaka na kuchota sh. 20,000 ndani ya sanduku.
Mmoja wa waumini wa kanisa hilo ambaye hakutaka jina lake kutajwa alisema licha ya muumini huyo kuondoka kiasi hicho, siku hiyo hiyo misa ya asubuhi alidakwa na Mashemasi wa kanisa hilo akichukua fedha isiyofahamika wakati alipoungana na waumini wengine kwenda kutoa sadaka, hata hivyo alisamehewa.
Mchungaji Gwamiye alithibitisha kutokea kwa tukio hilo kanisani kwake na kusema kwamba kumekuwepo na wimbi la vibaka wanaoingia ndani ya makanisa wakati maombi yakiendelea na kudokoa fedha za sadaka.
Katika tukio hilo Mchungaji Gwamiye alitoa wito kwa Makanisa ya Kipentekoste wilayani Kahama kukaa chonjo na vibaka wanaoingia makanisani na kujifanya ni waumini huku lengo lao likiwa ni kuvizia sadaka za waumini.
“Mtuhumiwa huyo alikamatwa na Mashemasi wakati walipomuona akiiba hela za sadaka baada ya kuanza maombi. Kama kiongozi wa kanisa hili nimemsamehe, lakini asithubutu kuingia katika makanisa yoyote hapa kahama maana waumini wakiamua kufunga novena ya maombi laana itamsumbua” alisema Gwamiye
Hata hivyo muumini huyo aliyejulikana kwa jina Dismas Simon mwenye umri wa miaka 35 alisema kuwa shetani ndiye aliyemtuma na kujikuta anaondoka na kiasi hicho cha fedha. Alimuahidi kiongozi huyo wa kanisa kuteua watu wa kuongozana nao kwa ndugu yake hali ambayo ilimfanya mchungaji amsamehe

0 Responses to “Muumini akamatwa akiiba sadaka kanisani ”

Post a Comment

More to Read