Thursday, June 5, 2014
SERIKALI YAENDELEA KUMKANA MASELLE
Do you like this story?
sakata la tuhuma za balozi wa uingereza nchini dianna Melrose limeendelea kuchukua sura mpya
na sasa mzigo huo unamwelema naibu
waziri wa nishati na madini stepheni maselle baada ya serikali kudai
kwamba ilikuwa ni kauli yake na si msimamo wa serikali .
Jana waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu uwekezaji na
uwezeshaji dk marry nagu alitoa kauli
bungeni kuwa kauli inayopaswa kufuatwa
kuhusu uhusiano baina ya Tanzania na
balozi huyo ni ili iliyotolewa na ikulu na si ya maselle
bungeni.
Nagu alitoa kauli hiyo kwa niaba ya waziri wan chi
ofisi ya waziri mkuu sera uratibu na
bunge na amesema katika hali ya kawaida
serikali inakuwa na kauli moja licha ya kuwa na vitengo vingi .
Nagu alitoa kauli ya serikali baada ya mwongozo wa
spika ulioombwa na mbunge wa kigoma kusini david kafulila ambaye litaka ufafanuzi kuhusu kauli tata.
Tofauti na miongozi mingine mwongozo huo ulitolewa majibu ya papohapo kwa naibu spika kumsimamisha dk nagu aliyekuwa amekalia kiti cha mratibu wa
shughuli za bunge
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


.gif)


0 Responses to “SERIKALI YAENDELEA KUMKANA MASELLE”
Post a Comment