Thursday, June 12, 2014
SERIKALI YAWATOA HOFU WANANCHI KUHUSIANA NA NDEGE ZA MALAWI ZINAZOONEKANA MKOANI MBEYA
Do you like this story?
SERIKALI
imesema kuwa ndege zinazoonekana mpakani mwa Tanzania na Malawi ni maalumu kwa
ajili ya kufanya utafiti na vyombo vya udhibiti wa anga vimezipa vibali vya
kuwa katika maeneo hayo.
Kauli hiyo
ilitolewa jana bungeni na Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe wakati
akijibu mwongozo wa Mbunge wa Ileje, Aliko Kibona (CCM), aliyetaka
ufafanuzi wa uwepo wa ndege hizo zinazoonekana zikizunguka katika wilaya za
Ileje na Kyela.
Akitoa
taarifa hiyo ya serikali, Waziri Mwakyembe alisema kuwa ndege hizo zipo
kihalali, hivyo aliwataka wananchi wa maeneo hayo kutokuwa na wasiwasi.
“Serikali
imejiridhisha kwamba hakuna ndege nyingine zaidi ya hizo za utafiti katika eneo
hilo la nchi. Kilichokosekana hapa Msheshimiwa Spika ni taarifa sahihi ndani ya
muda muafaka kwa wananchi, kuwa wategemee shughuli za kiutafiti za aina hiyo
katika maeneo yao,” alisema Waziri Mwakyembe.
Alizitaja
ndege hizo kuwa ni C-GSGJ Cessna 280, C-GSGL Cessna 280 na GSGL type 280
zinazofanya kazi ya kukusanya takwimu za kijiolojia nchini Malawi na zina
vibali vyote vya TCAA kuruhusu ndege hizo zinazoruka chini chini kugeuzia ndani
ya anga la Tanzania.
Ndege hizo
ni mali ya Kampuni ya Sander Geophysics (T) Limited, yenye makao makuu yake
Ottawa nchini Canada.
Aliwataka
wananchi kuendelea kutoa taarifa kwa vyombo vya dola pindi wanapoona matukio
yasiyo ya kawaida katika maeneo yao.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “SERIKALI YAWATOA HOFU WANANCHI KUHUSIANA NA NDEGE ZA MALAWI ZINAZOONEKANA MKOANI MBEYA”
Post a Comment