Thursday, December 18, 2014
ASHTAKIWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA KUCHANA NOTI YA SHILINGI 50
Do you like this story?
MWANAMUME alijipata taabani Alhamisi
alipofikishwa mahakamani kwa kurarua noti mbili za Sh50 baada ya kukosana na
kondakta wa matatu kuhusu nauli.
James Munene ambaye ni mhudumu wa bucha
mjini Ngong, alikamatwa na polisi kwenye barabara ya Ngong-Nairobi muda mfupi
baada ya kisa hicho cha Desemba 15.
Mahakama iliambiwa kuwa alimnyang’anya
kondakta Kenneth Thairu noti hizo na kuzirarua jambo ambalo ni kinyume cha
sheria za uhalifu nchini.
Shtaka lilieleza kuwa mshtakiwa
alikasirika Bw Thairu alipomwambia nauli ilikuwa Sh80 naye akasisitiza angelipa
Sh50.
Munene alimrukia na kumnyang’anya noti
hizo kisha akazirarua akisema zilikuwa zake na hakuna ambaye angemuuliza
chochote.
Hata hivyo, dereva wa matatu aliipeleka
katika kizuizi cha polisi wa trafiki kwenye barabara hiyo na mshukiwa akamatwa.
Alikabiliwa na shtaka la pili la
kumpiga Bw Thairu mdomoni na kumng’oa jino.
Ilidaiwa kuwa alitenda kosa hilo
alipomnyang’anya mlalamishi noti alizorarua.
Hata hivyo, alikanusha shtaka mbele ya
Hakimu Mkazi wa Kibera Bryan Khaemba aliyemwachilia kwa dhamana ya Sh30,000 na
dhamana sawa.
Hakimu alikataa kumwachilia kwa dhamana
ya pesa taslimu akisema kulingana na makosa yanayomkabili anaweza kutoroka.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ASHTAKIWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA KUCHANA NOTI YA SHILINGI 50 ”
Post a Comment