Thursday, December 18, 2014
MKUU WA WILAYA YA MAKETE AONGOZA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA KUKAGUA ENEO LILILOKUMBWA NA MADHARA YA UPEPO MKALI
Do you like this story?
Nyumba iliyobomolewa na mvua na upepo mkali |
Mkuu wa wilaya ya Makete akitoa maagizo baada ya kujionea hali halisi eneo la tukio |
Mkuu wa wilaya ya
Makete Josephine Matiro ametoa agizo kwa uongozi wa kata ya Matamba kufanya
mikutano ya kuwaelewesha wananchi umuhimu wa kujenga nyumba zao katika hali ya
uimara pamoja na kupanda miti ya matunda pembezoni mwa nyumba zao
Ametoa agizo hilo
hivi karibuni wakati alipotembelea eneo lililopata maafa ya kuezuliwa nyumba na
upepo mkali ulioambatana na mvua na kugundua kuwa ujenzi hafifu wa nyumba zao
nao umechangia kwa kiasi kikubwa hasara hiyo
"Wananchi
wanajenga nyumba hazina makoa, maeneo ni wazi hayana miti achilia mbali ya
matunda lakini hata mingine hakuna, haya maafa hayataisha, mtendaji nakuagiza
ufanye mikutano na wananchi na taarifa nipewe" alisema Matiro
katika tukio hilo
hakuna vifo wala majeruhi ya watu, zaidi ya nyumba na baadhi ya vitu
vilivyokuwa ndani kuharibika
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MKUU WA WILAYA YA MAKETE AONGOZA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA KUKAGUA ENEO LILILOKUMBWA NA MADHARA YA UPEPO MKALI ”
Post a Comment