Monday, December 29, 2014
NYALANDU ATANGAZA RASMI KUWANIA URAIS 2015
Do you like this story?
Mbunge wa Singida Kaskazini, Waziri wa Maliasili na
Utalii, Lazaro Nyalandu ametangaza rasmi kuwania Urais wa Tanzania katika
uchaguzi mkuu mwakani.
Amesema
amechukua uamuzi huo baada ya kuona kwamba anao uwezo wa kuiongoza Tanzania,
katika harakati za kuwafikisha kwenye maendeleo endelevu wanayotaka Watanzania.
Amesema, yuko
tayari kushindanishwa na Watanzania wengine watakaoona kuwa wanafaa kuwa Rais,
lakini akisema kwanza kila atakayejitokeza itabidi kazi zake zipimwe kwa moto
na endapo zitayeyuka hafai.
Nyalandu
ambaye alitangaza uamuzi huo kwenye Uwanja wa Michezo wa Ilongelo jimbo la
Singida Kaskazini, alisema, yeye anaingia kwenye kinyang’anyiro akiwa kifua
mbele kutokana na kuamini kwamba amekwishafanyakazi zilizotukuka.
“Kazi zangu
nilizofanya zinajulikana na ninaziamini kwamba ni nzuri, hivyo yeyote
atakayetaka urais apimanishwe na mimi kwa kupimwa kazi zetu kwa moto”, alisema
Nyalandu
Itakapofika
siku ya siku, nitaenda Dodoma nikisindikizwa na wana Singida Mashariki, na
wengine wengi kutoka pembe zote za Tanzania, kwenda Dodoma kuchukua fomu ya
kuwania kuteuliwa kugombea Urais kwa tiketi ya CCM”, alisema.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ NYALANDU ATANGAZA RASMI KUWANIA URAIS 2015 ”
Post a Comment