Wednesday, November 4, 2015
WANANCHI WAFANYA UHARIBIFU KATIKA BARABARA YENYE KIWANGO CHA KIMATAIFA JIJINI MBEYA
Do you like this story?
Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Nyilembe Munasa akiongea na wananchi wa isanga(Picha na David Nyembe wa Fahari News) |
Meneja wa Tanroads Mkoa wa Mbeya Mhandisi Paul Lyakurwa akitoa maelezo kwa wananchi wa Iganzo juu ya umuhimu wa alama za barabarani |
Moja kati ya Alama iliyokatawa na wananchi. |
Siku chache
mara baada ya kukamilika kwa ujenzi wa barabara Mbeya –Chunya yenye kilomita 72
ambayo inafadhiliwa na serikali kwa asilimia 100 kumeibuka kwa wizi wa
miundombinu ya barabara hiyo .
Baadhi ya
miundo mbinu iliyoibiwa katika barabara hiyo ni pamoja na alama za kuongozea
magari (road signs) pamoja na reli zilizowekwa kwenye kingo za barabra .
Akizungumza
na wananchi waishio kando ya barabara ya mbeya –chunya Mkuu wa
Wilaya ya Mbeya Nyilembe Munasa amesema mradi wa sehemu ya
kwanza Mbeya –Lwanjilo kilomita 36 ambao unatekelezwa na
makandarasi wa China communications construction company(CCCo) limited
kwa gharama ya shilingi bilioni 55 umeanza kuhujumiwa na watu wasio fahamika.
Amesema jumla
ya alama 43 za barabarani na reli zenye urefu wa mita 4 zimeibiwa katika
kipindi cha mwezi octobar mwaka huu ambazo thamani yake shilingi
milioni 6 .
Kufuatia hatua
hiyo Mkuu huyo wa wilaya ametoa wito kwa wananchi waishio pembezoni mwa
barabara hiyo ambao ni Isanga,Iganzo ,Mwansekwa na Ilowelo kuhakikisha wanakuwa
walinzi na watunzaji wa thamani zilizopo katika barabara hiyo.
Aidha mkuu huyo
wa wilaya ametumia fursa hiyo kuwataka wananchi hao kutofanya shughuli za
kilimo katika eneo la hifadhi ya barabara ambalo ni mita 30 kutoka katika
barabara kila upande kama ilivyo ainishwa kwenye sheria ya barabara Na 13 ya
2007.
Kwa upande wake
amesema kitendo kilichofanywa na watu hao ni aibu kubwa kwani mkoa mzima wa
mbeya barabara hiyo ndio pekee ilikuwa na alama zenye viwango vya kimataifa
hivyo hatuanhiyo imerudisha nyuma maendeleo ya mkoa.
Mwisho.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
1 Responses to “WANANCHI WAFANYA UHARIBIFU KATIKA BARABARA YENYE KIWANGO CHA KIMATAIFA JIJINI MBEYA”
November 5, 2015 at 10:37 AM
Isanga bhana,maendeleo ya kwetu wenyewe halafu mijitu inaibuka na kuibaaa miundo mbinu..........shame on us.
Post a Comment