Thursday, February 25, 2016
VIGOGO WALIOTOROSHA MAKONTENA KUANZA KUFILISIWA LEO
Do you like this story?
WADAIWA 16 waliokwepa kulipa kodi ya Mamlaka
ya Mapato Tanzania (TRA), baada ya kutorosha kontena za mizigo yao kwenye
Bandari Kavu (ICD) ya Azam mwishoni mwa mwaka jana, mali zao zinaanza kukamatwa
leo na kufilisiwa.
Mkurugenzi wa Mtendaji wa Kampuni ya Udalali
ya Yono, iliyopewa kazi ya kufuatilia wadaiwa hao wakiwemo baadhi ambao
wamekamilisha malipo, Yono Kevella alisema hayo Dar es Salaam jana.
Akizungumza na gazeti hili, Kevela alisema
kuanzia leo wanakaa na vyombo vya dola, kuanza utaratibu wa kukamata na
kufilisi mali za wahusika na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria.
Kevela alisema hadi sasa hakuna zuio
lililotolewa, linazowazuia kutekeleza wajibu wao katika kukusanya madeni hayo.
Hata hivyo alisema, wengi wa wadaiwa baada ya kutolewa kwa muda huo wa siku 14,
wameonesha moyo wa kulipa.
Wadaiwa 16 hawajamaliza madeni Alitaja
wadaiwa 16 ambao hawajalipa madeni yao wala kupunguza, ambao watafilisiwa
wasipojitokeza kufanya malipo ni Said Ahmed Said Sh 28,249,352.50, Strauss
International (45,393,769.95), Farid Abdallah Salum (52,185, 614.97).
Wengine ni Nasir Saleh Mazrui
(60,105,873.77), Simbo Yona Kimaro (64,221,009.10), Ally Masoud Dama
(102,586,719.22) na Juma Kassem Abdul (130,182,395.12), Salum Link Tyres (233,447,913.31)
na Tybat Trading Co.Ltd (448,690,271.90).
Pia wamo IPS Roofing Co.Ltd (966,723,692.10),
Tuff Tyres General Co Ltd, (7,435,254,537.03), Swalehe Mohamed Swalehe
(34,687,165.00), Rushwheel Tyre General Co Ltd, (1,802,988,679.20), Said Ahmad
Hamdan (68,362,558.31), Ahmed Saleh Tawred ( 59,237,578.40) na Farida Abdullah
Salem Sh 75,334,871. 85.
Akizungumzia wadaiwa waliolipa ndani ya siku
14 walizopewa na zikaisha juzi, alisema wanane kati ya 24, ndiyo walijitokeza
kulipa madeni baada ya kampuni yake kuwafuatilia.
Kevela alisema hadi jana zaidi ya Sh milioni
200 zimelipwa na wadaiwa hao.
Wadaiwa hao 24 walishindwa kulipa kodi kwa
wakati kama walivyotakiwa kufanya, ndipo TRA ilimpa dalali huyo kazi ya
kuwafilisi. Kampuni hiyo ya udalali ilitoa siku 14, kuanzia Februari 10, mwaka
huu wawe wamekamilisha; muda ambao umeisha juzi.
Kevela alisema katika siku hizo 14, kati
waliojitokeza kulipa,wanne kati yao wamemaliza madeni na wengine wanne
wamepunguza madeni na kuahidi kumalizia kiasi kilichobaki. Waliomaliza madeni
yao Wadaiwa waliolipa madeni yao yote ni Issa Ali Salim aliyekuwa akidaiwa Sh
94,543,161.96, Libas Fashion (26,593,245.78), Omary Hussein Badawy
(21,346,615.40) na Zulea Abas Ali (16,760577.24).
Waliopunguza madeni yao Waliopunguza madeni
yao ni Zuleha Abbas Alli aliyelipa Sh milioni 47 na kubakiwa na deni la Sh
28,508,551, awali alikuwa akidaiwa Sh 75,508,551.88, mwingine ni Ally Awes
Hamdani aliyelipa Sh milioni 17.26 awali alikuwa akidaiwa Sh 55,485,904.07).
Wengine waliopunguza kidogo ni Tifo Global
Trading Co Ltd waliolipa Sh milioni mbili ilhali deni lao ni Sh
1,573,300,644.58, Lotai Steel Tanzania Ltd, waliolipa Sh milioni mbili ilhali
deni lao ni Sh 5,476,475,738.19.
“Tulikabidhiwa wadaiwa 24 na TRA, waliokwepa
kodi kwa kutorosha kontena katika bandari kavu ya Azam mwishoni mwa mwaka jana,
sasa walipewa muda wa kulipa ila walikaidi, tukakabidhiwa tuwafilisi mali zao
zote ili kulipia madeni na wamejitokeza hao na kuanza kulipa wengine
wamemaliza”, alisema Kevela.
Awali wadaiwa 24, walikwepa kodi ya Sh
bilioni 18.95 kwa kutorosha makontena 329 ya bidhaa zao kutoka Kampuni ya SSB
ambayo ndiyo mmiliki wa bandari kavu ya (Azam ICD) na kampuni ya Regional Cargo
Services.
Mapema Desemba mwaka jana aliyekuwa Kaimu
Kamishna wa TRA, Dk Philip Mpango alizungumza na waandishi wa habari na kusema
kampuni 15 kati ya 43, zilizokwepa kodi baada ya kutorosha kontena 329 katika
ICD ya Azam, wamelipa.
Dk Mpango alisema Desemba 12, mwaka jana
ndiyo ilikuwa siku ya mwisho aliyotoa Rais John Magufuli ya siku saba kwa
wakwepa kodi hao 43, kulipa wenyewe kwa hiari, vinginevyo sheria zitachukua
mkondo wake. Kufuatia kauli hiyo ya Rais Magufuli, wadaiwa 15 walijitokeza na
kulipa na waliobaki hawakujitokeza kulipa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ VIGOGO WALIOTOROSHA MAKONTENA KUANZA KUFILISIWA LEO”
Post a Comment