Tuesday, February 23, 2016
WANANCHI WA MBEYA KUNUFAIKA NA UKUSANYAJI WA KODI.
Do you like this story?
Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya Dr Samweli Lazaro akichangia hoja. |
Mh Mbunge wa Songwe Filipo Mlugo akichakia hoja Juu ya Mkoa Mpya wa Songwe. |
Mh mbunge wa Ileje Janet Mbene pia akichangia katika kikao hicho( Picha na David Nyembe wa Fahari News) |
Wajumbe wakifatilia kwa makini |
NA SAMWEL NDONI, MBEYA.
MKUU wa mkoa wa Mbeya
Abbas Kandoro ameziagiza halmashauri zote za Wilaya na jiji kuelekeza nguvu
katika ukusanyaji na usimamizi wa mapato ya ndani ili kuondokana na utegemezi na
kufikia matarajio ya wananchi.
Akizungumza katika ufunguzi
wa kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa (RCC), cha mwelekeo
ya bajeti ya fedha kwa mwaka 2016/2017 amesema
halmashauri za mkoa wa Mbeya zimekuwa tegemezi kwa kiwango kikubwa.
Amesema kuwa takwimu
zinaonyesha kuwa utegemezi wa juu wa
halmashauri hizo ni asilimia 97 na utegemezi wa chini ni asilimia 76 na hivyo
uendeshaji wake kutegemea fedha kutoka nje.
Kandoro ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya RCC amesema kuwa
matarajio ya wananchi hayawezi kufikiwa bila halmashauri kuelekeza nguvu kwenye
ukusaji wa mapato.
Amesema uwezo wa
halmashauri katika kuwahudumia wananchi kwenye sekta mbalimbali ikiwemo elimu,
miundombinu na maji unategemea na mapato ya ndani yanayokusanywa.
Kikao hicho kimehudhuriwa
na wajumbe wa kamati ya ushauri kutoka mkoa wa Mbeya ambapo pamoja na mambo
mengine kinatarajia kujadili masuala mbalimbali pamoja na kuyawekea maazimio.
MWISHO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “WANANCHI WA MBEYA KUNUFAIKA NA UKUSANYAJI WA KODI.”
Post a Comment