Friday, March 4, 2016
BARCELONA YAVUNJA RECODI YA REAL MADRID ILIYOWEKWA MSIMU WA 1888/1889
Do you like this story?
Mabingwa wa Ligi Kuu ya Hispania (La Liga), Barcelona usiku wa kuamkia
Ijumaa wamefanikiwa kuvunja rekodi iliyowekwa na wapinzani wao wakubwa, Real
Madrid baada ya kupata ushindi wa goli tano kwa moja walpokuwa wakipamabana na
Rayo Vallecano.
Barcelona wamevunja rekodi ya kucheza michezo 35 bila kufungwa na kuipita
rekodi ambayo Madrid waliiweka ya kucheza michezo 34 bila kufungwa msimu wa
1888/1889 ambapo ni miaka 27 iliyopita.
Mchezaji bora wa mchezo huo alikuwa ni Lionel Messi abaye alifunga hat
trick katika dakika ya 23, 53 na 72, magoli mengine yalifungwa na Ivan Rakitic
dakika ya 22 na Arda Turan dakika ya 86 huku goli la kufutia machozi la Rayo
Vallecano likifungwa na Contreiras Gonçalves.
Aidha Rayo Vallecano ilimaliza mchezo huo ikiwa nusu baada ya wachezaji
wake wawili Diego Llorente dakika ya 42 na Manuel Iturra dakika ya 67
kuonyeshwa kadi nyekundu.
Baada ya matokeo hayo, Barcelona imefikisha alama 69 ikiwa katika nafasi
ya kwanza ya msimamo wa ligi hiyo ikifuatiwa na Atletico Madrid iliyo na alama
61, Rayo Vallecano wao wameshuka nafasi moja kutoka ya 16 hadi 17 na ikiwa na
alama 26.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ BARCELONA YAVUNJA RECODI YA REAL MADRID ILIYOWEKWA MSIMU WA 1888/1889”
Post a Comment