Saturday, March 5, 2016
BOMU LALIPUKA ZANZIBAR, WANANCHI WAINGIWA NA HOFU
Do you like this story?
Kukiwa kumesalia wiki mbili kabla ya marudio ya uchaguzi mkuu
Zanzibar wakaazi wa maeneo ya michenzani na walio karibu na maeneo hayo
wamekumbwa na hofu kubwa baada ya bomu kulipuka usiku wa kuamkia leo na
kuzua tafrani kubwa.
Bomu hilo ambalo hadi sasa halijathibitishwa kama ni la
kivita au la kutengenezwa hapa nchini limelipuka katika eneo la Maskani ya CCM
ya Kisonge na kuharibu Kontena kubwa la Maskani hiyo na kupasua vioo vya
madirisha ya baadhi ya nyumba za maendeleo za michenzani ,hata hivyo
hakuna mtu aliyeumia na kulipuka kwa bomu hilo na Kontena hilo lilikuwa
tupu.
blog hii ilifika katika eneo hilo na kushuhudia askari wa
upelelezi wa jeshi la polisi wakiwa katika harakati za upelelezi na kukusanya
vitu amabvyo huenda vikawa vinahusiana na kulipuka kwa bomu hilo,mmoja wa
kijana aliyejitambulisha kwa jina la Shababi Said Mtamanya amedai
kuwoana baadhi ya watu wakiwa na gari dogo lawazi wengine wakiwa
wamefunika nyuso zao katika eneo hilo la Kontenna na baadaaye kuondoka kwa
mwendo wa kasi.
Wakti polisi wakiendelea na uchuguzi wao makamu wa pili wa
Rais balozi Seif Ali Iddi alifika katika eneo hilo na kukagua na
kuangalia athari za kulipuka kwa bomu hilo ambapo akizungumza na itv amesema
seriklai inalaani kitendo hicho amabacho kinahatarisha amani ya nchi h
uku akiahidi serikali itaendelea kuhakikisha hali ya amani na utulivu
inaendelea.
Naibu mkurugenzi wa upelelezi na makosa ya jinai Zanzibar
kamishna msaidizi Salum Msangi akiongea amesema polisi imeshaanza kazi yake kwa
asilimia 70 na kutoa onyo kali.
Hili ni tukio la kwanza la Ulipuaji wa mabomu kwa mwaka 2016
wakati Zanzibar ikijiandaa kwa uchaguzi wa marudio machi 20 mwakaa huu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ BOMU LALIPUKA ZANZIBAR, WANANCHI WAINGIWA NA HOFU”
Post a Comment