Wednesday, March 2, 2016
MAFUTA YASHUKA BEI, ZIPO HAPA BEI MPYA.
Do you like this story?
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetangaza bei
kikomo za mafuta ya aina ya Petroli, Mafuta ya Taa na Diseli.
Akizungumza na waandishi wa habari, Mkurugrnzi Mkuu wa EWURA, Felix
Ngamlagosi amesema mafuta ya Petroli yamepungua kwa shilingi 31, Dizeli
imepungua kwa shilingi 114 na Mafuta ya Taa kwa shilingi 234.
Ngamlagosi alisema bei mpya zinaanza kutumika leo Machi, 2 sasa Dar es
Salaam mafuta ya Petroli itauzwa 1,811, Dizeli 1,486 na Mafuta ya Taa 1,465.
Aidha alisema kuwa bei kwa mkoa wa Tanga haitapungua kutokana na bandari
ya mkoa huo kutokupokea mafuta mapya katika bandari hiyo na hivyo wataendelea
kutumia bei za mwezi Februari.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ MAFUTA YASHUKA BEI, ZIPO HAPA BEI MPYA.”
Post a Comment