Wednesday, March 9, 2016

SERIKALI YA TANZANIA NA AFRIKA KUSINI ZAKUBALIANA KUBADILISHANA UZOEFU KATIKA SEKTA YA FILAMU


Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akifurahi jambo na Balozi wa Afrika kusini nchini Tanzania Bw.Thamsanga Mseleku alipomtembelea ofisini kwake jijini Dar es Salaam.Katika maongezi yao wamekubaliana kushirikiana katika masuala ya sekta ya filamu na hasa katika kubadilishana uzoefu katika mambo ya haki miliki na Sera.



Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo zimekubaliana kubadilishana uzoefu na mafunzo katika masuala ya filamu, haki miliki na Sera.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye alipokuwa akiongea na balozi wa afrika kusini nchini ofisini kwake jijini dar es Salaam.

Waziri nape amemwomba balozi uyo nafasi hiyo kwa sababu afrika kusini ipo vizuri zaidi na mbali katika sekta ya filamu na kwayo itakuwa nafasi nzuri kwa nchi izi mbili kukaa pamoja ili wabadilishane uzoefu na hasa suala la haki miliki na sera,kwani serikali yetu iko mbioni kutengeneza sera madhubuti ili sekta hii ya filamu iwe rasmi.

Alieleza kuwa ili tusonge mbele hatuna budi kuangalia kwa wenzetu wanafanyaje ili litatuongezea ujuzi na maarifa wakati tunajipanga na mengine kwani wageni sasa wameanza kuingia Tanzania kwa kuwa inafanya vizuri katika sekta hii ya filamu na ivyo ni wajibu wetu kuhakikisha tunatengeneza sera na mazingira madhubuti ili wakija wasiondoke.

Kwa upande wake Balozi wa Afrika kusini nchini Tanzania Bw. Thamsanga Mseleku ameishukuru serikali yake kuendelea kuimarisha mahusiano baina yao na amehaidi kufanikisha makubaliano ya kukutanisha wasanii kutoka afrika kusini na wa Tanzania ili wabadilishane uzoefu ili watoe kazi zenye viwango bora Zaidi ili kazi zao zifike mbali.

Makubaliano haya yamekuja baada ya wasanii wa filamu Single Mtambalike na Elizabeth Michael kushinda Tuzo katika Africa magic Viewer’s choice Awards na walipomtembelea ofisini kwake  walimwomba waziri uyo mwenye dhamana kuwasaidia kutengeneza Sera madhubuti ili sekta hii iwe rasmi na wanufaike na jasho lao.
Imeandaliwa na Daudi Manongi.

0 Responses to “ SERIKALI YA TANZANIA NA AFRIKA KUSINI ZAKUBALIANA KUBADILISHANA UZOEFU KATIKA SEKTA YA FILAMU”

Post a Comment

More to Read