Wednesday, March 9, 2016
SERIKALI YA TANZANIA NA AFRIKA KUSINI ZAKUBALIANA KUBADILISHANA UZOEFU KATIKA SEKTA YA FILAMU
Do you like this story?
Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo
zimekubaliana kubadilishana uzoefu na mafunzo katika masuala ya filamu, haki
miliki na Sera.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape
Nnauye alipokuwa akiongea na balozi wa afrika kusini nchini ofisini kwake
jijini dar es Salaam.
Waziri nape amemwomba balozi uyo nafasi hiyo kwa sababu afrika kusini ipo
vizuri zaidi na mbali katika sekta ya filamu na kwayo itakuwa nafasi nzuri kwa
nchi izi mbili kukaa pamoja ili wabadilishane uzoefu na hasa suala la haki
miliki na sera,kwani serikali yetu iko mbioni kutengeneza sera madhubuti ili
sekta hii ya filamu iwe rasmi.
Alieleza kuwa ili tusonge mbele hatuna budi kuangalia kwa wenzetu
wanafanyaje ili litatuongezea ujuzi na maarifa wakati tunajipanga na mengine
kwani wageni sasa wameanza kuingia Tanzania kwa kuwa inafanya vizuri katika
sekta hii ya filamu na ivyo ni wajibu wetu kuhakikisha tunatengeneza sera na
mazingira madhubuti ili wakija wasiondoke.
Kwa upande wake Balozi wa Afrika kusini nchini Tanzania Bw. Thamsanga
Mseleku ameishukuru serikali yake kuendelea kuimarisha mahusiano baina yao na
amehaidi kufanikisha makubaliano ya kukutanisha wasanii kutoka afrika kusini na
wa Tanzania ili wabadilishane uzoefu ili watoe kazi zenye viwango bora Zaidi
ili kazi zao zifike mbali.
Makubaliano haya yamekuja baada ya wasanii wa filamu Single Mtambalike na
Elizabeth Michael kushinda Tuzo katika Africa magic Viewer’s choice Awards na
walipomtembelea ofisini kwake walimwomba waziri uyo mwenye dhamana
kuwasaidia kutengeneza Sera madhubuti ili sekta hii iwe rasmi na wanufaike na
jasho lao.
Imeandaliwa na Daudi Manongi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ SERIKALI YA TANZANIA NA AFRIKA KUSINI ZAKUBALIANA KUBADILISHANA UZOEFU KATIKA SEKTA YA FILAMU”
Post a Comment