Wednesday, March 9, 2016
SERIKALI YAWAPA MOTISHA WACHEZAJI WA TIMU YA TAIFA WANAWAKE" TWIGA STARS"
Do you like this story?
Serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imetimiza
ahadi yake ya kuwapa motisha wachezaji wa timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu
wanawake “Twiga Stars” kwa kuwapa kila mmoja shilingi Laki tatu taslimu
kutokana na kufanikiwa kutikisa nyavu za Zimbabwe licha kutoibuka na ushindi.
Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
Annastazia James Wambura wakati wa mkutano wake na wachezaji hao jijini Dar es
Salaam.
Wambura alisema pamoja na Twiga Stars kufungwa kwa magoli 2-1 bado
mmejitahidi sana katika ukilinganisha na miaka ya nyuma ambapo kwenye
mashindano kama hayo walikuwa wanafungwa hadi magoli matano kwa sifuri.
Aliongeza kuwa kutokana na jitihada hizo anatimiza ahadi yake ya kumpatia
kila mchezaji kiasi cha shilingi 300,000/= fedha ambazo anaamini zitawazidishia
hari na morali ya ushindi katika mchezo wa marudiano.
“Kutoka na na jitihada zenu mlizozionyesha wakati wa mchezo huo ninatoa
kwa kila mchezaji kiasi cha shilingi 300,000/= na ahadi hii inaendelea
tena katika mchezo wa marudiiano” Alisema Naibu Waziri.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Wanawake Tanzania
(TWFA) Amina Karuma alitoa wito kwa wachezaji kuhakikisha katika mechi ya
marudio wanashinda kwa hari na mali ili kuonyesha thamani umuhimu wao
Aidha alitumia fursa hiyo kuwaomba wadau wa michezo kuendelea kujitokeza
kusaidia maendeleo ya michezo hasa Soka la wanawake kwani kumekuwa na
changamoto ya wafadhili hali inayopelekea kusuasua.
Motisha hiyo kwa wachezaji imetokana na michango ya wadau mbalimbali
awalioguswa na timu hiyo wadau waliochangia mpaka sasa ni TCRA (10,000,000/=),
ASAS(2,000,000/=), Mohamed Enterprises (2,000,000/=) na mdau ambaye akupenda
jina lake litajwe (3,000,000/=) na kufanya mpaka sasa kuwa na jumla ya shilingi
milioni 17.
Kwa wadau wanaopenda kuchangia watumie Akaunti namba 20110001677 Twiga Stars Special Fund NMB Bank House, kwa wale wanaotaka kuchangia
vifaa waiwasilishe Wizarani mtaa wa Ohio Jengo la Golden Jubilee Ghorofa ya
nane.
Imetumwa na Frank Shija, WHUSM
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “SERIKALI YAWAPA MOTISHA WACHEZAJI WA TIMU YA TAIFA WANAWAKE" TWIGA STARS"”
Post a Comment