Wednesday, March 9, 2016
TRA YAFUTA KODI ELEKEZI KWA WAFANYABIASHARA
Do you like this story?
Kaimu Kamishna wa TRA, Alphayo Kidata akifafanua jambo waandishi wa habari (Hawapo pichani) kuhusu mpango wa Serikali kuwasaidia wananchi wa kipato cha chini ili waweze kumudu kulipa kodi |
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imefuta kodi elekezi kwa bidhaa
zinazoingizwa nchini kwa msamaha wa kodi hususani zile zinazotoka nchini China
kwa kuwata wafanyabiashara wanaoagiza na kuingizi bidhaa kutoka huko kulipa
kodi inayotakiwa.
Hayo yamesemwa leo na Kaimu Kamishna wa TRA, Alphayo Kidata alipokuwa
akizungumza na waandishi wa habari katika utaratuibu wa kuongea na umma kwa
kuwapa taarifa kuhusu makusanyo ya kodi ya kila mwezi.
Kaimu Kamishna huyo amesema kuwa Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato
Tanzania imeamua kufuta kodi elekezi ambayo ilikuwa inawapa punguzo la kodi
wafanyabiashara wanaoagiza na kuingiza bidhaa toka nchini China kwa kupunguziwa
sehemu ya kodi.
“Tumeamua kuondoa kodi elekezi kwasababu haina faida kwa taifa letu kwani
inawanyima wafanyabiashara wengine ambao hawaagizi bidhaa kutoka China fursa ya
kushindana kibiashara na Serikali yetu sio ya kibaguzi ndio maana tumaeamua
kufuta kodi hii ili kuleta usawa kwa wafanyabiashara wote nchini”Alisema
Kidata.
“Suala liliopo kwa sasa ni kwa kila mwananchi anayepaswa kulipa kodi
katika kitu anachokifanya alipe kodi na atutafumbia macho ukwepaji wa kodi na
hakuna kitu kinachoitwa kodi elekezi wala msamaha wa kodi katika Serikali hii,
tulipe kodi kwa maendeleo ya taifa letu” aliongeza Kidata.
Aidha, Kamisha Kidata amesema kuwa hakuna Sheria yoyote inayosema kuwa
kutakuwa na kodi elekezi ama msamaha wa kodi kwa mfanyabiashara yoyote yule
bali ule ulikuwa ni utaratibu tu uliowekwa na Mamlaka na baada ya
kuona hauna umuhimu wala faida katika nchini yetu ikaamriwa ufutwe.
Katika kusisitizi suala la kufutwa kodi elekezi na utekelezaji wake Kaimu
Kamishna wa kodi za Ndani toka TRA, Salum Yusuf amesema watalisimamia suala la
ulipaji kodi na yeyote atakayekaidi kulipa kodi kwa Mamlaka husika
watawachukulia hatua za kisheria na kusisitiza kuwa kulipa kodi ni jukumu la
kila mtanzania katika kuleta maendeleo ya taifa letu.
Mamlaka ya Mapato Tanzania imekuwa na rekodi nzuri ya ukusanyaji wa kodi
tangu mwezi Desemba mwaka 2015 kwa kukusanya zaidi ya shillingi trillioni 1 na
wanaendelea na kasi ya kukusanya kodi zaidi na kwa takwimu zilizopo kuanzia
mwezi Julai mwaka 2015 mpaka mwezi Februari mwaka huu wamekusanya jumla ya
shillingi trillioni 8.6 ikiwa ni asilimia 99 ya malengo waliojiwekea.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ TRA YAFUTA KODI ELEKEZI KWA WAFANYABIASHARA”
Post a Comment