Sunday, March 13, 2016

ZIARA YA SIKU MBILI YA NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI MKOANI MBEYA.


Naibu waziri wa Tamisemi Mhe. Suleiman Jaffo akizungumza mara Baada ya kutembelea Guba( Dampo) la kisasa lililopo Nsalaga ambalo muda sio mlefu litaanza kutumika.(Picha na David Nyembe wa Fahari News)

Mwonekano wa Guba ( Dampo) lililopo Nsalaga jijini Mbeya

Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya Dt. Samweli Lazaro akitoa ufafanuzi wa Ujengwaji wa Dampo hilo la kisasa kwa Naibu waziri wa Tamisemi Mhe. Suleiman Jaffo.(Picha na David Nyembe wa Fahari News)

Mwonekano wa Machinjio Mpya ya N"gombe ambayo yataanza kutumika hivi karibuni yaliopo katika Wilaya Mpya ya songwe Eneo la Utengule.


Naibu waziri wa Tamisemi Mhe. Suleiman Jaffo alifanya Ziara katika Hospitali ya Mkoa jijini Mbeya kujionea utendaji wa kazi na changamoto Mbalimbali.



Naibu waziri wa Tamisemi Mhe. Suleiman Jaffo akiangalia Barabara za mradi wa Benki kuu ya dunia.




Naibu waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) mhe. Suleiman Jaffo yuko jijini Mbeya katika ziara yake ya kikazi ya siku mbili ambapo katika siku yake ya kwanza amefanya ziara katika hospitali ya mkoa wa Mbeya, Shule ya sekondari ya Iyinga Tech pamoja na guba (dampo) la kisasa la jijini Mbeya na mradi wa barabara za benki kuu ya dunia.

Katika ziara hiyo naibu waziri, mh. Jaffo alianzia katika shule ya sekondari ya Iyunga Tech ambayo hivi karibuni imekumbwa na majanga mawili ya moto mfululizo na kusababisha hasara kuaffobwa za mali za wanafunzi na shule hiyo.

Mhe. Jaffo ametoa pole baada ya kutokea majanga hayo ya moto katika shule ya Iyunga Tech na kuahidi kusimamia ukarabati wote wa shule hiyo mpaka itakapokuwa katika hali ya kawaida  huku akipongeza jitihada zinazofanywa ili kulifanyia kazi agizo lake la kukarabatiwa mapema shule hiyo ili ifikapo tarehe mosi mwezi ujao wa Aprili wanafunzi watakaporejea shuleni wakute mazingira mazuri ya kusomea.

Pamoja na hayo mhe. Jaffo ametoa agizo kwa hospitali ya mkoa wa Mbeya kuhakikisha wanapata kiwanja kilichopo karibu na hospitali hiyo ili ijengwe mara moja hospitali maalumu ya wakina mama wenye matatizo mbalimbali, pia amepongeza utendaji kazi wa hospitali hiyo na na kutatua changamoto zilizo chini ya watendaji wa hospitali hiyo ya mkoa wa Mbeya.

Aidha mhe. Jaffo ametembelea mradi uliokamilika wa guba la kisasa ambalo litahudumia wakazi wote wa halmashauri ya jiji la Mbeya.

Ziara ya naibu waziri wa TAMISEMI mhe. Suleiman Jaffo anaendelea na ziara leo ikiwa ni siku ya pili ya ziara hiyo hapa mkoani Mbeya ambapo atatembelea soko jipya la Mwanjerwa na baadae jioni atazungumza na wafanyakazi wote wa mkoa wa Mbeya.

0 Responses to “ZIARA YA SIKU MBILI YA NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI MKOANI MBEYA.”

Post a Comment

More to Read