Wednesday, August 31, 2016
BABA MZAZI WA DIDA AAGWA RASMI LEO
Do you like this story?
Leo tarehe 31, Agosti 2016 ndio
ilikuwa siku maalumu kwa Viongozi wa Serikali, Viongozi wa Soka nchini, wachezaji
pamoja na watu mbalimbali kumuaga marehemu baba mzazi wa golikipa wa Timu ya
Taifa ‘Taifa Stars’ na timu ya Young Africans ‘ Yanga’ Deogratus Bonventure
Munishi ‘Dida.
Katika kumuaga marehemu mzee
Bonventure Munishi walijitokeza watu mbalimbali wakiwemo mwenyekiti wa Yanga
Yusuph Manji, makamu wa Rais wa Simba Geofrey Nyange Kaburu na wachezaji soka
mbalimbali akiwemo golikipa wa zamani wa Timu ya Taifa ambaye pia aliwahi
kuichezea klabu ya Yanga Ivo Mapunda.
Baba mzazi wa Dida, marehemu Mzee
Munishi alifariki tarehe 28 Agosti, 2016 ambapo mazishi ya mzee Munishi yatafanyika
Kibosho Mkoani Kilimanjaro.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


.gif)




0 Responses to “BABA MZAZI WA DIDA AAGWA RASMI LEO”
Post a Comment