Monday, September 12, 2016
UKAWA WALALA MBELE MECHI YA WABUNGE
Do you like this story?
Mambo
hayajaisha? Ndivyo unavyoweza kujiuliza baada wabunge wanaounda Umoja wa Katiba
ya Wananchi (Ukawa) kususia mechi ya mpira wa mguu kati ya timu ya wabunge na
Kamati ya Amani ya viongozi wa dini wa Mkoa wa Dar es Salaam.
Wabunge
hao wamesusia mchezo huo kwa madai kuwa kuna ajenda ya siri kwenye mchezo huo.
Kutokana
na uamuzi huo, badala ya viongozi hao wa dini kucheza na timu ya Bunge,
walicheza na timu ya maveterani ya Dodoma, huku taarifa nyingine zikidai kuwa
wabunge wamezuiwa kushiriki.
Wakizungumza
kwa nyakati tofauti mjini Dodoma, wabunge wa Ukawa wamesema wameacha kwenda
kucheza baada ya kutoshirikishwa katika maandalizi ya mechi hiyo.
Mbunge
wa Mbozi (Chadema), Pascal Haonga amesema hawakuenda uwanjani kwa sababu kamati
hiyo ilialikwa na Naibu Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson ambaye wamekuwa na
mgogoro naye kwa muda mrefu.
Mwenyekiti
wa Timu ya Bunge, Willam Ngeleja alipotafutwa simu yake iliita bila majibu.
Hata
hivyo, siku moja kabla ya kuchezwa kwa mechi hiyo Ngeleja alikaririwa na
Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) akisema mchezo huo ulilenga kuenzi amani
kwa Watanzania.
Hata
hivyo, Naibu Spika Dk Tulia Ackson amesema wabunge wengi hawakuwepo katika
mechi hiyo kwa sababu ni mwisho wa wiki na wengine wameenda mashambani na
wengine majimboni.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


.gif)

0 Responses to “UKAWA WALALA MBELE MECHI YA WABUNGE”
Post a Comment