Thursday, December 15, 2016
ALIYETAKA KUMUUA DONALD TRUMP AHUKUMIWA KWENDA JELA
Do you like this story?
Mwanamme mmoja raia wa Uingereza
amehukumiwa kifungo cha miezi 12 jela kufuatia jaribio lake la kutaka kunyakua
bunduki kwa lengo la kumuua Donald Trump.
Michael Sandfgord mwenye umri wa miaka 20 alikiri makosa hayo ya
kumiliki bunduki na kuvurua mkutano.
Analaumiwa kwa kujaribu kunyakua bunduki kutoka kwa polisis wakati
wa mkutano wa hadhara huko Las Vegas ili kumfyatulia risasi mgombea urais.
Mahakama ilisema kuwa huenda akaachiliwa baada ya miezi minne
ambapo atasafirishwa hadi nchini Uingereza
Baada ya Sandford kukamatwa aliwaambia maafisa kuwa alikuwa na
mpango wa kumpiga risasi Donald Trump.
Hata hivyo hakufanikiwa kunyakua bunduki kutoka kwa afisa wa
polisi.
Mamake alisema kuwa alikuwa amepoteza mawasiliano na mwanawe,
ambaye aliondoka nyumbani kutembea kote marekani mwaka 2015.
Kulingana na nyaraka za mahakama Sandfords ambaye hakuwa na makao
na ambaye alikuwa akiishi Marakani kinyume na sheria baada ya muda wa visa yake
kuisha, aliiwaambia majasusi kuwa aliendesha gari kutoka California hadi Nevada
kwa lengo la kumpiga risasi Trump.
Anaripotiwa kumuambi afisa wa polisi kuwa alitarajia kuuawa kwenye
shambulizi hilo na kwamba alikuwa na tikiti za kuhudhuria mkutano mwingine wa
Trump baadaye ikiwa angapata fursa ya pili.
Majaji walitaja kitendo hicho kuwa cha kustaajabisha.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ALIYETAKA KUMUUA DONALD TRUMP AHUKUMIWA KWENDA JELA”
Post a Comment