Monday, December 5, 2016
WAZIRI JAFFO ATOA SIKU 4 KWA MIKOA YOTE NCHINI
Do you like this story?
MIKOA yote Tanzania Bara
imepewa siku nne kuhakikisha inatoa idadi ya vituo vya afya vitakavyoingizwa
kwenye mfumo wa ukusanyaji wa mapato ya Serikali za Mitaa kwa njia ya
kielektroniki.
Agizo hilo limetolewa leo
na Suleiman Jaffo, Naibu Waziri wa Nchi, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(TAMISEMI) na kwamba, mpaka sasa sasa vituo 65 pekee kati ya 5511 ndivyo
vilivyofungiwa mfumo huo.
Jaffo amesema hayo wakati
wa ufunguzi wa mafunzo ya kuwajengea uwezo timu ya wawezeshaji wa kitaifa wa
mfumo wa ukusanyaji mapato wa serikali za mitaa kwa njia ya kielektronik
GoT-HoMIS na LGRCIS.
Mafunzo hayo yameandaliwa
na wataalamu kutoka Shirika la Elimu Kibaha na Chuo Kikuu Mzumbe wakishirikia
Kurugenzi ya Uimarishaji Mifuko ya Sekta za Umma (PS3) kwa ufadhili wa Shirika
la Misaada la Marekani (USAID) yaliyofanyika Chuo Kikuu Mzumbe mkoani humo.
Amesema serikali ilifanya
uamuzi wa kuwa na mfumo mmoja wa kielektroniki wa Teknolojia ya Habari na
Mawasiliano (TEHAMA) ulioandaliwa na wataalamu hao utakaotumika katika
kusimamia, kuboresha na kuimarisha utoaji wa huduma bora za afya.
Lakini pia ukisaidia
ukusanyaji mapato hasa katika menejimenti ya upokeaji na utoaji wa madawa na
vifaa tiba na shughuli zingine za sekta ya afya kama ilivyo kwenye mfumo wa
mapato wa LGRCIS.
Amesema mikoa mingi
haijafanya vizuri katika kutoa idadi ya vituo vya afya na hivyo kujikuta kila
mkoa ukiwa chini ya asilimia 10 jambo linaloleta maana tofauti katika mikoa
husika kwenye suala nyeti kama hilo.
“Hatuwezi kwenda kama
tunafanya mambo kwa mazoea na haiwezekani mkoa ukaleta idadi ya vituo chini ya
vituo 10 katika mkoa, hapo sitawaelewa,” amesema Jaffo.
Jaffo amewataka viongozi
kuwa wasimamizi wazuri katika matumizi ya mifumo hiyo ya kielektronik kufuatia
tabia iliyojionesha awali ya uwepo wa baadhi ya vituo kutumia njia ya
kielektronik kwa muda mfupi na baadaye kuacha na kuhamia kwenye vitabu kwa
maslahi yao binafsi.
Amesema
kwamba, ukusanyaji wa mapato hayo kwa njia ya kielektronik una lengo zuri la
kuboresha makusanyo kufuatia mikoa iliyojaribiwa kuonesha mafanikio.
Ametolea
mfano Mkoa wa Mwanza katika kituo cha Kololeni ambapo awali makusanyo yalikuwa
ni Sh. 4.8 Mil na sasa ni Sh. 6 Mil.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “WAZIRI JAFFO ATOA SIKU 4 KWA MIKOA YOTE NCHINI”
Post a Comment