Thursday, March 27, 2014
BUNGE LA KATIBA LIVUNJWE KIKWETE AMEMALIZA KAZI.
Do you like this story?
Siasa ni kama mchezo ambao kanuni zake
zinaweza kuitofautisha na soka; mchezo ambao hauhitaji waamuzi watatu uwanjani
ili uchezeshwa kwa haki.
Haishangazi, hata hivyo kuona siasa ikiitwa mchezo
mchafu ambao kanuni za uchezeshaji wake ndizo zinazoweza kuibua hisia zikiwamo
za kutokuwapo kwa haki katika uchezeshaji wake.
Mchakato wa kuandikwa kwa Katiba Mpya nchini
ambao ulianza Aprili 6, 2012 kwa Rais Jayaka Kikwete kutangaza Tume ya
Mabadiliko ya Katiba chini ya uongozi wa Jaji Joseph Warioba ikiwa ni
kutekeleza ahadi yake kwa Watanzania kuwa angewapatia Katiba Mpya umefikia
patamu, ingawa umeacha pia maswali mengi.
Bunge la Katiba linaloendelea mjini Dodoma
wiki jana lilishuhudia mambo kadhaa ambayo yameacha wengi vinywa wazi.
Kitu kisichotarajiwa na kilichowashangaza
wengi ni Rais Kikwete kuhutubia Bunge hilo Ijumaa akiwa tayari na majibu ya
baadhi ya vipengele vya Rasimu ya Pili ya Katiba mkononi mwake ikiwamo muundo
wa Muungano.
Kutokana na hotuba hiyo, inawezekana Rais
Kikwete hakuwa tayari kupokea maoni tofauti na msimamo wake na chama chake, CCM
ambao ni serikali mbili.
Kwa upande wao, wachambuzi wa masuala ya
siasa nchini wanahoji kama ni hivyo, ilikuwaje Kikwete akatumia Sh75 bilioni za
kodi za Watanzania kuandaa mchakato ambao tayari alikuwa na majibu
yake?
Msomi na mchambuzi wa masuala ya siasa kutoka
Chuo Kikuu cha Mzumbe, Profesa George Shumbusho anasema Rais Kikwete ‘ametibua’
mwenendo wa mchakato kwani kama alikuwa ana hoja zake, alitakiwa kutumia nafasi
yake kujadiliana na tume hiyo badala ya kutoa maoni yake mbele ya Bunge hilo.
“Alitakiwa kusimama kama mkuu wa nchi kuwa
tofauti na msimamo wowote kwa kutoa mwelekeo wa kuchambua rasimu badala ya kutoa
maoni yake, kufanya hivyo ni kupinga wazi kwamba kilichopendekezwa ndani ya
rasimu ni makosa,” anasema na Profesa Shumbusho.
“Kutokana na hotuba hiyo sioni haja ya
kuendelea na mchakato huo, kama serikali mbili ndiyo zinahitajika kwa hivyo ni
vyema Bunge livunjwe na tuanze upya mchakato, vinginevyo hakuna
kitakachoendelea”.
Kwa upande wake, Profesa Bonaventure
Rutinwa kutoka Shule Kuu ya Sheria, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam anasema tatizo
lililojitokeza katika uwasilishaji wa hotuba ile ni pamoja na kujenga dira na
imani ya mawazo yake kuwa ni sahihi, hivyo kuathiri uhuru na mawazo ya wajumbe
waliyokuwa nayo awali.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “BUNGE LA KATIBA LIVUNJWE KIKWETE AMEMALIZA KAZI.”
Post a Comment