Wednesday, March 26, 2014
BWANA YESU ASIFIWE YAMKERA KINGUNGE.
Do you like this story?
Mjumbe wa bunge la katiba
kingunge ngombale mwiru amesema salamu
za wanasiasa zinamkera kwa kuwa wanafanya wasilolijua.
Salamu iliyomkera kingunge ni kwa baadhi ya watu kusema “Bwana
yesu asifiwe” au “Tumsifu yesu
kristo” ambazo alisema ni salamu za
kitumwa lakini akasifia salamu ya
Assalaam Aleykum.
Kingunge ambaye
anajulikana kama muumini mkubwa wa siasa
ya ujamaa alitoa kauli hiyo katika semina
ya waandishi wa habari kuhusu
wajibu wao katika kuripoti bunge la katiba iliyoandaliwa na Baraza la Habari Tanzania (MCT).
Mkongwe huyo ni mmoja wa
watu ambao wasio na imani ya dini na mara zote
amejipambanua kuwa haamini hilo
na hata katika viapo vyake hatumii
kitabu chochote cha dini.
“Salamu ya ‘bwana Asifiwe’
Au Tumsifu yesu kristo ni matokeo ya utumwa
ambayo mimi nimekuwa nikikerwa
hasa kwa wanasiasa ambao wanapenda
kuitumia alisema kingunge.
“Sisi tangu zamani tunajua
kuwa Assalam Aleykum ni amko la amani ambalo lilikuwepo kabla ya mtume kuliko hizo nyingine ambazo hata ndani ya CCM
wanafanya hivyo wakidhani ni sahih”
Salmu hiyo hutumiwa na
waumini wa kikristo lakini pia katika mikutano mbalimbali ya kisiasa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “BWANA YESU ASIFIWE YAMKERA KINGUNGE.”
Post a Comment